GARETH BALE AFIKIA MAKUBALIANO MASLAHI BINAFSI NA REAL MADRID

Gareth Bale amefikia makubaliano ya maslahi binafsi na Real  Madrid kuelekea uhamisho utakaovunja rekodi ya dunia kutoka  Tottenham.
Pamoja na hilo lakini miamba ya soka ya kihispania bado kwenye mazungumzo ya mwisho na Spurs juu ya ada ya uhamisho wa  £86m .
"Wakati mazungumzo yakiendelea jijini Madrid, tayari mchezaji ameshakubaliana maslahi binafsi na klabu," amesema mwandishi mkuu wa habari za

0 comments:

KWELI NIJANGA LA KITAIFA SHULE KUKOSA WANAFUNZI

 
Takwimu zilizotolewa juzi na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kuhusu wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano katika sekondari za Serikali na vyuo vya ualimu mwaka huu zinasononesha na zimethibitisha pasipo kuacha shaka kwamba nchi yetu inaelekea kuzimu katika suala zima la elimu.
   Hatuhitaji kupiga ramli kujua

0 comments:

ULINZI SHIRIKISHI WATUMIKA KUTAPELI KITUO KIKUU CHA MABASI UBUNGO

 
Hali ya usalama kwenye Kituo Kikuu cha Mabasi yaendayo Mikoani (UBT), imekuwa tete baada ya kuibuka kwa kundi kubwa la matapeli wanaowaibia abiria na kuwabambikizia kesi kwa kutumia njia ya ulinzi shirikishi.
Mbali na kufanyika kwa vitendo hivyo kituo hicho kinadaiwa kuwa soko kubwa la biashara haramu ya dawa za kulevya aina ya Bangi na Mirungi.
Kundi hilo ambalo linajulikana kama vishoka limekuwa likifanya vitendo hivyo kuanzia saa mbili usiku kwa kujifanya kuwa wao ulinzi shirikishi, na kufanya utapeli huo kwa kuwakamata abiria na baadhi ya watu wanaoingia kwenye kituo hicho na kuwapa makosa mbalimbali.
Uchunguzi uliyofanywa na gazeti hili takriban siku tatu kwenye kituo hicho majira usiku na mchana, umebaini kwamba mchezo huo mchafu umekuwa ukifanyika kwa muda mrefu ambapo tayari kundi kubwa la watu wametapeliwa na kuibiwa vitu mbalimbali.
Uchunguzi huo umebaini kwamba moja ya utapeli unaofanywa na kundi hilo la vijana wanaojiita ulinzi shirikishi, ni kutumia pete feki za dhahabu ambazo wanazitumia kuwatapeli fedha abiria.
Pia, licha ya kufanya utapeli huo kwa kutumia dhahabu feki, kundi hilo linatumia bidhaa ya sabuni kuwatapeli simu abiria. Sabuni hutengenezwa kwa mfano wa simu na kuwabambika watu kuwa ni simu halisi.
Licha ya kufanyika kwa vitendo hivyo, uchunguzi pia umebaini kuwepo

0 comments:

WAANDISHI WAPINGA CHADEMA KUJENGA MNARA WA MWANGOSI

CHAMA cha Waandishi wa Habari Mkoani Iringa (IPC), kimepinga ujenzi wa mnara katika Kijiji cha Nyololo kwenye eneo alilofia Mwenyekiti wa zamani wa chama hicho Daudi Mwangosi unaotakiwa kutekelezwa na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Mwenyekiti wa IPC, Frank Leonard alisema Chadema wameazimia kujenga mnara huo bila kuwashirikisha waandishi wa habari jambo ambalo kamwe halitaunga mkono.

Alisema IPC haiungi mkono suala hilo kwa vile Mwangosi alikuwa kazini alipopatwa na maafa hayo.

Leonard amesema si vema siasa ikaingia kwenye kumbukumbu za kifo cha kiongozi wao.

“Msimamo wetu kama chama kutokana na bodi yetu tunapinga asilimia 100 azimio la Chadema kujenga mnara wa mwandishi mwenzetu bila kutushirikisha.

“Sisi kama chama hatujaafiki hilo kwa sababu kazi wanayofanya ilitakiwa ifanywe na waandishi wa habari hivyo ilitakiwa tuwaalike sisi na siyo wao watualike,”alisema.

Alisema Chadema wanaamini kuwa marehemu Mwangosi alikuwa mkereketwa wao ingawa wanahabari hawaamani jambo hilo.

Leonard alisema ni hatari kutumia

0 comments:

CHADEMA WANATAKA KUVUNJA UNDUGU NA MSHIKAMANO WA WATANZANIA'' NGOMBALE MWIRU


Ngombale Mwiru, amepingana wazi wazi na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kuhusu rasimu ya Katiba mpya. Mwanasiasa huyo, ambaye ametumikia Serikali kwa nyadhifa mbalimbali na katika vipindi tofauti pamoja na chama hicho kikuu cha

0 comments:

KICHWA CHA MTUI CHAPATIKANA NJEE YA OFISI YA MWENYEKITI TUME YA TAIFA YA POLISI KENYA

 Kenya's police commission chairman Johnston Kavuludi (file photo) 
Polisi nchini Kenya wanachunguza kisa ambacho kichwa cha mtu aliyeuawa kilipatikana kimewekwa nje ya afisi ya mwenyekiti wa tume ya kitaifa ya polisi Johnston Kavuludi jijini Nairobi.
Kifurushi hichi kilichokuwa kimefungwa kwa karatasi ya plastiki, vilevile kilikuwa na mikono miwli ya binadamy iliyojaa damu.
kando ya kifurishi hicho kulikuwa na ilaani iliyoandiskwa ''Kavuludi wewe ndiye utakayefuata''.
Tangu uteuzi wake, kamishna huyo

0 comments:

MAREKANI BADO YASISITIZA KUIADHIBU SYRIA

 
Marekani imedhihirisha wazi kuwa itaiadhibu Syria kwa shambulio la Damascus ambapo zaidi ya watu 1,400 waliuawa huku wachunguzi wa umoja wa Mataifa wakikamilisha uchunguzi wao na kuondoka Syria leo (31.08.2013).
Rais wa Marekani Barrack Obama amesema hawawezi kukubali ulimwengu ambao unaruhusu wanawake, watoto na raia wasio na hatia kuuawa katika kiwango kikubwa.
Obama amesema Marekani bado inapanga hatua za kijeshi lakini hajaeleza ni lini hasa hatua hizo zitachukuliwa.Matamshi yake yanakuja huku nchi yake ikitoa ripoti ya kijasusi inayoonyesha utawala wa Syria ulishambulia eneo karibu na mji mkuu Damasacus na kuwaua watu 1,429 wakiwemo watoto 426.
Obama amesema ulimwengu una wajibu wa kuhakikisha kuwa hakuna matumizi ya silaha za kemikali na kulishutumu baraza la usalama la umoja wa mataifa kwa kushindwa kuafikiana kuhusu hatua gani ichukuliwe dhidi ya Syria.
Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani John Kerry hapo jana alizungumza

0 comments:

MANDELA HAKUTOLEWA HOSPITALI BADO MAHTUTI JAPO HALI YAKE IMETULIA KIDOGO

Serikali ya afrika Kusini imekanusha taarifa za vyombo vya habari kwamba aliyekuwa kiongozi wa afrika Kusini, Nelson Mandela, ambaye amelazwa hospitali tangu mwezi wa Juni, kwamba alirejeshwa nyumbani Johannesburg Ijumaa usiku.
Taarifa ya serikali imesema

0 comments:

TUHUMA ZA SYRIA KUTUMIA SILAHA ZA KEMIKALI NI UPUUZI MTUPU'' RAIS VLADIMIR PUTIN WA URUSI


Putin
Rais Vladimir Putin wa Urusi anasema tuhuma kuwa serikali ya Syria ilitumia silaha za kemikali ni upuuzi mtupu.
Anasema jeshi la Syria lilikuwa linasonga mbele, hapakuwa na sababu ya serikali kuwapa kisingizio wale wanaotaka kuingia kijeshi.
Bwana Putin alisema ikiwa Marekani ina ushahidi kuthibitisha tuhuma zake, basi ikabidhi ushahidi huo kwa Baraza la Usalama la Umoja wa

0 comments:

RAYC AOKOKA NAKUBATIZWA KANISA LA SILOAM JIJINI DAR

MSANII wa Kizazi kipya nchini, Rehema Chalamila ‘Ray C’, ameamua kuokoka na kumrudia Mungu na kubatizwa katika Kanisa la Siloam, jijini Dar es Salaam. Ray C alikuwa akipatiwa tiba kutokana na kuathirika na utumiaji wa dawa za kulevya, ikiwa ni msaada kutoka kwa Rais Jakaya Kikwete.

Akizungumza jana Dar es Salaam kwa simu, Ray C alisema ameamua kumrudia Mungu na kuachana na mambo ya kidunia kutokana na mengi

0 comments:

''VIONGOZI WA CCM WANAFIKI WAMEJAA CHUKI TUPU''MANSOUR

 
Siku saba tangu Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (Nec), kumvua uanachama, Mwakilishi wa Jimbo la Kiembesamaki, Mkoa wa Mjini Magharibi, Mansour Yussuf Himid, kutokana na kukiuka miiko ya chama hicho, ameibuka jana na kukiponda chama hicho kuwa kimejaa siasa za chuki na ubaguzi.
Huku akizungumza kwa umakini na kujiamini alisema, “ CCM kimejaa ubaguzi, siasa za chuki na kimeshindwa kusimamia misingi imara ya kutetea masilahi ya wananchi. Wazanzibari kataeni hali hii, wekeni tofauti za vyama pembeni, Zanzibar kwanza vyama baadaye.

0 comments:

MAN UTD, L'POOL LEO HAPATOSHI ANFIELD


London, England. Kocha David Moyes ataiongoza Manchester United kuifuata Liverpool kwa mara ya kwanza leo kwenye Uwanja wa Anfield, huku Arsenal wakiwakaribisha Tottenham Spurs.
Moyes aliondoka Everton na kuchukua mikoba ya Sir Alex Ferguson msimu huu, lakini sasa anarejea Merseyside ikiwa ni baada ya michezo mitatu msimu huu.
Kikosi chake cha United kimekuwa na matokeo ya kuvutia wakishinda moja, sare dhidi ya Chelsea Jumatatu.
“Anfield ni sehemu ngumu wakati wote,” alisema Moyes. “Ni uwanja mzuri nimejiandaa kurudi hapo, najua hali inavyokuwa unapocheza kwenye uwanja ule ni wazi mechi itakuwa ngumu na ushindani kama inavyokuwa wakati wote, ni matumaini yangu tutaondoka

0 comments:

MAREKANI INAJIPANGA KUINGILIA KIJESHI SYRIA

 
Marekani inaendelea kusaka "Muungano wa kimataifa" katika maandalizi yake ya kuishambulia Syria ikibidi, kutokana na tuhuma za serikali ya nchi hiyo kutumia gesi ya sumu dhidi ya raia.
Tuanzie lakini nchini Syria kwenyewe ambako wataalamu wa Tume ya Uchunguzi ya Umoja wa Mataifa wanatarajiwa kuyatembelea kwa mara ya mwisho hii leo yale maeneo ya karibu na mji mkuu Damascus yanayosemekana gesi za sumu zilitumika na kuangamiza maisha ya

0 comments:

ISRAELI KUWASAFIRISHA WAHAMIAJI WA KIAFRIKA MPAKA UGANDA

Israel hivi karibuni ina mipango ya kuanza kuwarejesha barani Afrika wahamiaji takribani 50,000 kutoka Eriteria na Sudan.Inaaminika wahamiaji hao watapelekwa Uganda
Taarifa kutoka kwa waziri wa ndani wa Israel Gideon Sa'ar imesema hivi karibuni itaanza harakati za kuwarejesha barani Afrika wahamiaji ambao wengi waliingia nchini humo tangu mwaka 2006 kupitia Misri ambayo inapakana na Israel.
Israel inawaona wahamiaji hao kuwa wageni waliongia kinyume cha sheria, na inasema wameleta kero katika maeneo masikini nchini humo wakitafuta nafasi za kazi. Aidha Israel imepuzilia mbali msimamo wa mashirika ya kutetea haki za binadamu kuwa wengi wa

0 comments:

WAASI WA M23 WATANGAZA KUSITISHA MAPAMBANO

 Waasi wa M23 mashariki mwa DRC
Kundi la waasi wa M23 katika Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo limesema kuwa linasimamisha mapigano mara moja, kuruhusu uchunguzi juu ya makombora yaliyovuka mpaka na kuanguka katika nchi jirani ya Rwanda.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Lambert Mende, ameiambia DW mjini Kinshasa kuwa serikali ya nchi hiyo haijashangazwa na hatua hiyo ya M23, lakini akasisitiza kuwa wanachotaka wao ni kuona waasi hao wakiweka silaha chini, kama wanavyotakiwa na jumuiya ya kimataifa na pia serikali ya Kongo.
Jana, Rwanda ililishutumu jeshi la Jamhuri ya

0 comments:

HAKIKA ARSENAL WANA KIBARUA KIZITO ULAYA...NA MAN CITY, UNITED, CHELSEA NAZO...

MSIMU uliopita walipokutana kwenye Uwanja wa Emirates na wana fainali ya Ligi ya Mabingwa, Oktoba 22, matokeo yalikuwa Arsenal 0 Borussia Dortmund 0.
Lakini nje ya Uwanja, matokeo mengine yanaleta habari nyingine tofauti.
Kuingia fainali msimu uliopita Uwanja wa

0 comments:

ETO'O ATAMBULISHWA RASMI CHELSEA NA KUKABIDHIWA UZI WA BLUU

MSHAMBULIAJI Samuel Eto'o amesainisi Mkataba wa mwaka mmoja na Chelsea jana kwa mshahara wa Pauni Milioni 7 kwa mwaka.
Mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 32 ametambulishwa rasmi leo baada ya kukamilisha vipimo vya afya.
Mwanasoka huyo bora mara nne Afrika ambaye aliwasili London juzi usiku kwa treni kutoka Ufaransa hadi Stesheni ya St.

0 comments:

CHEKA AMMSHUSHA BONDIA WA MAREKANI ILINGONI

 
HATA hivyo pambano hilo pamoja na yale ya utangulizi yaliingia dosari baada ya wachezaji kama Alfonce Mchumiatumbo, aliyekuwa akizichapa na Chupac Chipindi katika pambano lao la utangulizi la raundi sita, kugoma kupanda ulingoni kwa kile walichokuwa wakieleza mabondia hao kuwa wanahitaji kumaliziwa pesa zao za mkataba wa kucheza mechi hizo kabla ya kupanda ulingoni. 
 
Nao mabondia Mada Maugo na Thomas Mashali, pia waligoma kupanda ulingoni wakishinikiza kumaliziwa pesa zao kwanza jambo ambalo lilifanya kuzua taflani ukumbini hapoa huku mapambano yakich

0 comments:

WANAUME WATAKIWA KUFUNGA UZAZI IWAPO WANAISI WAMEPATA WATOTO WAKUTOSHA

 
Ni nadra kwa wanaume kukubali kufunga uzazi, lakini waliofanya hivyo wameona mafanikio yake.
Sumbawanga. “Baada ya kupata mtoto wa nne nilidhani mke wangu asingeweza tena kushika mimba kutokana na umri aliokuwa nao, lakini nilishangaa baada ya kukaa miaka kumi akapata ujauzito na ndipo nilipoamua kwenda kufunga uzazi,”anasema Bevin Mtendo (55).
Mtendo, ambaye ni Mkuu wa Idara ya Usafi wa Mazingira Wilaya ya Sumbawanga Mkoa wa Rukwa amekuwa kivutio kikubwa kwenye jamii tangu alipoamua kufunga uzazi mwaka 2008 kutokana na wanaume wengi kumfuata kuomba ushauri.
Anasema ana watoto watano na kwamba mtoto wa mwisho alimpata baada ya miaka kumi baada ya kudhani kuwa mke wake asingeweza kuzaa tena.
Anasema kabla ya kufunga uzazi, mke wake alikuwa akitumia njia za kisasa za uzazi wa mpango, lakini baada ya kujifungua mtoto wa nne aliacha na kudhani kuwa hawezi kupata tena ujauzito.
Hata hivyo, anasema baada ya miaka kumi kupita mkewe alipata ujauzito hali iliyomlazimu yeye kuamua afunge uzazi.
“Tulijua hatuwezi kupata tena mtoto, lakini alipokuja huyu wa tano

0 comments:

KIKWETE AMUOMBA MUSEVENI KUMALIZA MGOGORO WA RWANDA NA TANZANIA

Mgogoro wa kidiplomasia ulioibuka kati ya Rwanda na Tanzania, jana ulitinga bungeni huku Rais Jakaya Kikwete, akimuomba Rais wa Uganda, Yoweri Museveni kuwa msuluhishi wa mgogoro huo.
Hata hivyo, Kiongozi wa Kambi rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe alionyesha kutoafiki kuombwa kwa Rais Museveni akisema naye yuko katika kundi linaloitenga Tanzania.
Kauli ya kwamba Tanzania kupitia kwa Rais Kikwete imemuomba Rais Museveni kuwa msuluhishi wa mgogoro huo,ilitolewa jana bungeni na Waziri Mkuu Mizengo Pinda. Waziri Mkuu alikuwa akijibu swali la papo kwa hapo aliloulizwa na Mbowe akitaka kupata kauli

0 comments:

SUMU YA NYUKI YAGUNDULIKA KUWA DAWA INAYOWEZA KUANGAMIZA VIRUSI VYA UKIMWI


Wengi tunafuga nyuki, tunakula asali lakini hatujui kama nyuki wana faida zaidi ya hizi hapa.
Wanasayansi kutoka chuo kikuu cha tiba Washington, Marekani  wamegundua katika utafiti wao kuwa sumu iliyopo katika mwili wa nyuki iitwayo toxin melittin inaweza kuvivunjavunja na kuviharibu virusi vya Ukimwi pasipo kuacha madhara katika chembehai za mwili.
Habari hii imeelezwa katika taarifa ya tiba za dawa za kupunguza makali ya virusi vya Ukimwi iliyotolewa mapema mwaka huu.
Watafiti hawa wanaeleza kuwa matokeo ya utafiti huu kufika katika hatua kubwa inayoleta matumaini ya kupamba na VVU  kwa kuweza kupata dawa ya kupaka ya majimaji ndani ya uke itakayotumika kupambana na maambukizi ya VVU.
Dk Joshua Hood anasema: “Matumaini yetu ni kwa maeneo ambayo hali ya maambukizi yapo juu na vigumu kuzuilika, dawa ya majimaji mazito inaweza kutumika kupaka ndani

0 comments:

IGP ASAFISHA VIGOGO UWANJA WA NDEGE BAADA YA KUBUKA KASHFA ZA MADAWA YA KULEVYA

 
Siku chache baada ya kuibuliwa kwa kashfa ya kupitishwa kiholela kwa dawa za kulevya katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), Jeshi la Polisi limemwondoa Kamanda wa Polisi wa Viwanja vya Ndege Kamishna Msaidizi (ACP), Deusdedit Kato pamoja na Mkuu wake wa Upelelezi, David Mwafwimbo.
Mbali ya maofisa hao, pia jeshi hilo limemwondoa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Linus Sinzumwa, naye ikiwa ni miezi michache baada ya kutokea kwa ghasia wakati baadhi ya wakazi wa huko walipokuwa wakipinga mpango wa Serikali wa ujenzi wa bomba la gesi kwenda Dar es Salaam.
Nafasi ya Kamanda Sinzumwa imechukuliwa na Kamishna Msaidizi

0 comments:

UKUAJI WA UCHUMI AFRIKA SASA WAWA FUMBO KWA VIONGOZI WA AFRIKA

 epa02803364 This handout image made available by Government Communication and Information System Republic of South Africa (GCIS) shows shows (front row L-R) President of Burkina Faso Blaise Compaore, President of Chad Idriss Deby, President of Congo Denis Sassou , President of Algeria Abdelaziz Bouteflika at the official opening ceremony of the 17th Ordinary Session Of The Assembly Of The African Union at Sipopo Conference Centre in Malabo, Equatorial Guinea, 30 June 2011. The theme of the Summit is 'Accelerating Youth Empowerment for Sustainable Development' which runs from 23 June to 01 July 2011. EPA/NTSWE MOKOENA HANDOUT HANDOUT EDITORIAL USE ONLY/NO SALES
Afrika inasherehekea miaka 50 ya umoja wa kisiasa na uchumi unaonawiri, ambapo bara hilo kwa muda mrefu sasa linaangaliwa kama eneo la neema kubwa, licha ya ukuaji huo wa kiuchumi kuwa na walakini.
Bara la Afrika linasherehekea hivi sasa miaka 50 ya Umoja wa Afrika kwa ufanisi tangu wa kisiasa mpaka wa kiuchumi. Bara hilo linajitokeza kama eneo lenye fursa kubwa ya kuwavutia wawekezaji. Baada ya "Chui wa Asia" sasa Simba wa Afrika wananguruma.
Takwimu zinadhihirisha uchumi utakuwa mwaka huu kwa 7% au zaidi katika robo ya mataifa yote ya eneo la kusini mwa jangwa la Sahara. Wakati huo huo, mengi ya mataifa hayo yamo katika lile kundi la mataifa ambayo uchumi wake unakuwa haraka kupita kiasi.
Waafrika wawili kati ya watano wana simu ya mkononi au Smartphone. Nguvu za ununuzi zinazidi kukuwa barani Afrika na masoko yanaongezeka, huku matajiri wakizidi kuongezeka barani humo. Huu ni ufanisi wa kusisimua ambao watu wanapenda kuuzungumzia – naiwe wanasiasa, wanauchumi na pia vyombo vya habari.
“Afrika inajikwamua“, anasema mwandishi habari wa masuala ya kiuchumi Anver Versi. Mkenya huyo anaemiliki jarida la kiuchumi la African Business Magazine linalochapishwa mjini London anasema: "Kuna sababu nzuri za kuhoji kwamba Afrika itageuka kuwa soko muhimu la ukuaji wa kiuchumi katika miaka 50 inayokuja .Kwa sababu Afrika ina mali ghafi na nguvu kazi. Mtu anaweza kusema Afrika ni mahala pa kuvutia kabisa kuwekeza hivi sasa - Wachina wameitambua hali hiyo tangu miaka 10 au 15 iliyopita. Na sasa wajasiriamali wa Kijerumani na wazungu kwa jumla wanabidi wazindukane na kuitambua fursa hiyo."
Matumaini yana walakini
Katuni ya maadhimisho ya miaka 50 ya Umoja wa Afrika. Katuni ya maadhimisho ya miaka 50 ya Umoja wa Afrika.
Kwa mujbu wa makadirio ya Benki Kuu ya Dunia, uchumi katika eneo la kusini mwa jangwa la Sahara utakuwa kwa kadiri ya 5% katika kipindi cha mwaka 2013 na 2015. Uchumi wa dunia katika kipindi hicho hicho utakuwa kwa kadiri ya 3% tu.
“Viwango hivyo ni vya juu vya ukuaji wa kiuchumi, lakini hiyo bado si sababu ya kushangiria,“ anasema Robert Kappel. Mtaalam huyo wa Kijerumani anayeshughulikia masuala ya utafiti wa masuala ya Afrika katika taasisi ya GIGA mjini Hamburg, amechunguza makadirio ya ukuaji wa kiuchumi katika mataifa 42 ya kusini mwa jangwa la Sahara. Mengi ya mataifa hayo hayatofua dafu kwa mlinganisho wa kimataifa.
Robert Kappel anasema: "Ukuaji unatokana zaidi na ile hali kwamba mahitaji ya mali ghafi na bidhaa za mashambani yameongezeka sana katika kipindi cha miaka iliyopita na kwa namna hiyo bei nazo zimepanda. Kwa hivyo, inamaanisha biashara ya nje inachangia sana katika ukuaji wa kiuchumi barani Afrika na huo ni udhaifu mkubwa."
Taasisi kuu za fedha duniani, Shirika la Fedha la Kimataifa na Benki Kuu ya Dunia, zote zinaonya juu ya bara la Afrika inategemea sana biashara na nchi za nje. Naye Katibu Mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa, Kofi Annan, aliyataka mataifa ya viwanda katika Kongamano la Kiuchumi la Kimataifa hivi karibuni mjini Cape Town nchini Afrika ya Kusini yawekwe sheria kali katika biashara ya mali ghafi pamoja na Afrika. “Rushwa na kukwepa kulipa kodi za mapato,“ anasema Kofi Annan, “ndio chanzo cha kudhoofika neema barani Afrika.“
Nini cha kufanya kuimarisha uchumi?
Mchoro wa maadhimisho ya miaka 50 ya Umoja wa Afrika. Mchoro wa maadhimisho ya miaka 50 ya Umoja wa Afrika.
Shughuli za viwanda zinazorota barani Afrika na kilimo hakitoshi hata kukidhi mahitaji ya wakaazi wa bara hilo. Hata katika soko la ajira hakuna ishara ya kuongezeka nafasi za kazi. Hata katika nchi inayonyanyukia kiuchumi ya Afrika ya Kusini, zaidi ya 25% ya wakaazi wake hawana kazi na wanaoathirika zaidi ni vijana wanaoishi mashambani.
Kwa hivyo, nini cha kufanya ili ukuaji wa kiuchumi barani Afrika utuwame katika msingi imara? Mwandishi habari wa masuala ya kiuchumi, Anver Versi, anahisi panahitajika vitega uchumi zaidi katika miundo mbinu. Naye Robert Kappel wa Taasisi ya Uchunguzi wa Masuala ya Afrika anahisi mageuzi ya kiuchumi pia yanahitajika pamoja na sheria bora za uwekezaji ili kuwavutia wateja tangu wa ndani mpaka wa kimataifa.
Mwandishi: Julia Hahn/MMD Regionen Afrika

0 comments:

ENNAHDA YASEMA IKO TAYARI KUTOA TAHFIFU TUNISIA

 Rached Ghannouchi, leader of the Islamist Ennahda movement, speaks during a news conference in Tunis August 15, 2013. The chairman of Tunisia's ruling Islamist party rejected on Thursday opposition demands for a non-party government, saying this could not steer the country through the delicate situation it is in. Ghannouchi said he would accept the creation of a government of national unity, but only provided all political parties are represented. REUTERS/ Zoubeir Souissi (TUNISIA - Tags: POLITICS CIVIL UNREST)
Chama cha Kiislamu kinachotawala nchini Tunisia kimeashiria kuwa tayari kujadiliana na upinzani kuhusu kuundwa kwa serikali isiyo ya wanasiasa, ili kukomesha mgogoro wa kisiasa uliyodumu kwa mwezi mmoja sasa.
Chama cha Kiislamu kinachotawala nchini Tunisia kimeashiria kuwa tayari kujadiliana na upinzani kuhusu kuundwa kwa serikali isiyo ya wanasiasa, ili kukomesha mgogoro wa kisiasa uliyodumu kwa mwezi mmoja sasa.
Tangazo la kile ambacho kinaweza kuwa tahfifu muhimu ambayo Ennahda imepinga hadi wakati huu, lilifuatia mkutano wa mwenyekiti wa chama hicho Rachid Ghanouchi, na Haoucine Abassi, katibu mkuu wa chama cha wafanyakazi chenye nguvu UGTT, ambacho kimechukua jukumu la

0 comments:

OPERESHENI YA KIJESHI YANUKIA SYRIA BILA UN

  The US aircraft carrier Carl Vinson (R) and the cruiser USS Bunker Hill (L) sit anchored off Manila Bay after arriving on May 15, 2011 for a four-day port of call accompanied by three other warships. The Carl Vinson is making a port call in the Philippine capital after its crew buried Osama bin Laden's remains in the Arabian Sea AFP PHOTO / JAY DIRECTO (Photo credit should read JAY DIRECTO/AFP/Getty Images)
Uwezekano wa Umoja wa Mataifa kuidhinisha mashambulizi dhidi ya Syria ni mdogo sana, lakini tayari Marekani na washirika wake wanafanya maandalizi ya mashambulizi kupitia dhana ya uwajibikaji wa kimaadili.
Wiki moja baada kutokea shambulio linalodaiwa kuwa la kemikali n

0 comments:

NI LINI MAREKANI ITAISHAMBULIA SYRIA?

 Rais Barack Obama wa 
Marekani.
Rais Barack Obama wa Marekani amesema Jumatano (28.08.2013) bado hajasaini mpango wa kuishambulia Syria lakini kuna uwezekano wa kuchukuliwa hatua hiyo baada ya Marekani kuashiria haitohitaji ruhusa ya Umoja wa Mataifa.
Shutuma za kisiasa nchini Uingereza zimeweka mashaka iwapo Uingereza itaweza kujiunga na hatua ya kijeshi ya Marekani kuiadhibu serikali ya Rais Bashar al Assad wa Syria kutokana na shambulio lake la silaha za sumu iwapo hatua hiyo ya kijeshi itachukuliwa kabla ya wi

0 comments:

ETO'O ATUA KWA 'GOGO' LONDON TAYARI KUKAMILISHA USAJILI WAKE CHELSEA

KLABU ya Chelsea itamsaini Samuel Eto’o kwa Mshahara wa Pauni Milioni 7 kwa mwaka leo Alhamisi baada ya kukubali matokeo ya kumkosa mshambuliaji wa Manchester United, Wayne Rooney.
Eto’o, mshambuliaji wa Cameroon mwenye umri wa miaka 32 amekubali malipo hayo kidogo kutoka Pauni Milioni 17 alizokuwa akilipwa Anzhi Makhachkala kwa mwaka na kumfanya awe mchezaji anayelipwa zaidi duniani na atasaini kama mchezaji huru.
Pamoja na hayo, inafahamika Anzhi imemlipa mamilioni Eto’o ya Pauni ili kuvunja naye Mkataba.
Full steam ahead: Samuel Eto'o arrived at St Pancras station on Wednesday night ahead of his move to Chelsea
Kifaa kinawasili: Samuel Eto'o akiwasili Stesheni ya Treni ya St Pancras jana usiku tayari kukamilisha uhamisho wake Chelsea
Whisked away: Eto'o leaves St Pancras after arriving in London
Whisked away: Eto'o leaves St Pancras after arriving in London
Ndani ya Treni: Eto'o, anayetarajiwa kupata mshahara wa chini Chelsea, akiwa ndani ya Treni baada ya kutua St Pancras jana usiku
Solution? Samuel Eto'o will seal his move to Chelsea as Jose Mourinho ends his striker search
Suluhisho? Samuel Eto'o anatua Chelsea kumaliza tatizo la safu ya ushambuliaji kwa Jose Mourinho
Top target: Mourinho didn't select any strikers at Old Trafford and is known to be chasing Wayne Rooney
Mlengwa: Mourinho amemkosa Wayne Rooney wa Man United

REKODI ZA MAGWIJI CHELSEA KABLA YA SAMUEL ETO'O

Chelsea imewahi kusaini wachezaji wakongwe kabla ya Eto'o na imepata matokeo tofauti. . .
George Weah
Mchezaji bora zaidi daima Afrika alitua mwaka 2000 kutoka AC Milan, akiwa na umri wa miaka 33. Hakupewa nafasi sana chini ya kocha Gianluca Vialli, licha ya kufunga bao katika mchezo wake wa kwanza na Spurs. 
MATOKEO: Alifeli.
Gianfranco Zola
Alitua London mwaka 1996 akiwa na umri wa miaka 30 na katika mechi 312 alifunga mabao 80, na kujitengenezea heshima kubwa darajani.
MATOKEO: Alifanikiwa.
Gianluca Vialli
Akiwa na umri wa miaka 32-alikataa kujiunga na Rangers na kusaini kikosi cha Ruud Gullit mwaka 1996. Lilikuwa dau kubwa la Pauni 600,000 na Vialli akaenda kufunga mabao 40 katika mechi 78, kisha akaeukia kuwa kocha mwenye mafanikio. 
MATOKEO: Alifanikiwa.
Pop Robson
Gwiji huyo wa Newcastle na West Ham alijiunga na Chelsea akiwa na umri wa miaka 36 mwaka 1982. Alifunga katika mechi yake ya kwanza, lakini akafunga mabao mawili tu zaidi akiwa kocha na mchezaji. 
MATOKEO: Alifeli.
Andriy Shevchenko
Milan ilisikitika wakati Sheva anaondoka akitimiza miaka 30 kwa dau la Pauni Milioni 30.8. Lakini mashabiki wa Chelsea muda si mrefu walijutia usajili wa mshambuliaji huyo wa Ukraine, ambaye aliishia kufunga mabao 22 katika misimu mitatu.
MATOKEO: Alifeli.
Eto'o aliwasili katika Stesheni ya Treni ya London, St Pancras usiku wa jana na anatarajiwa kufanyiwa vipimo katika viwanja vya mazoezi vya Chelsea, Cobham kabla ya kukamilisha usajili wake leo.
Kocha wa Chelsea, Jose Mourinho, alithibitisha kumfanya Eto’o mchezaji wa pili anayemzikia na mpango wake B baada ya United kugoma kumuuza Rooney.
Kwa sasa, mshambuliaji huyo wa England ameamua kuendelea na maisha Old Trafford baada ya kuandika katika ukurasa wake wa Facebook kuwashukuru mashabiki kwa mapokezi mazuri wakati United ikimenyana na Chelsea na kutoa sare ya bila kufungana usiku wa Jumatatu.
Rooney aliposti: "Ilikuwa vigumu kuamini namna mashabiki walivyofanya, nawashukuru mno. Hakika nakubali sapoti yenu. Inamaanisha mengi,".
Mourinho anaweza kujaribu tena baadaye msimu huu kuinasa saini ya Rooney, lakini kwa sasa anamaliza shida zake kwa Eto’o, ambaye aliwahi kumzungumzia kwamba: "Kocha yeyote atakuwa mpumbavu kutotaka kuwa na mshambuliaji kama yeye,".
Kuna mambo makubwa yanatarajiwa kutokana na kocha huyo wa Chelsea na mchezaji wake huyo mpya.
Eto’o hajawahi kwenda tofauti na matarajio. Akiwa Barcelona, alikamata kipaza sauti katika matangazo ya moja kwa moja ya Televisheni na kuikandia klabu yake ya zamani, Real Madrid ‘b*****ds’ kushangilia taji la Barcelona la ubingwa wa Hispania mwaka 2005; aliwahi pia kuponda hadharani kiwango cha chini cha Ronaldinho na aliwahi kuondoka uwanjani baada ya mashabiki jukwaani kuanza kumfanyia hila za kibaguzi katika mechi na Zaragoza.
Ajabu pamoja na urafiki wake na Mourinho kwa sasa, lakini wametokea kuwa adui kiaina fulani.
Alipokwenda Stamford Bridge mwaka 2005 wakati Chelsea ilipoifunga Barcelona katika Ligi ya Mabingwa, Eto’o alitoa maoni yake akikandia mbinu za kiuchezaji za Chelsea. Mourinho anapenda uimara wa mchezaji huyo.
"Nilipenda ukweli kwamba anafanya kazi kwa kujituma,"alisema Mourinho.
Wawili hao baadaye waliuangana Inter Milan ambako Eto’o alimuwezesha Mourinho kushinda mataji matatu ndani ya msimu. Wakati huo, Mwanasoka huyo bora mara nne Afrika alifunga bao pekee la ushindi Stamford Bridge na kumaliza matumaini ya Chelsea katika Ligi ya Mabingwa.
Reunion: Eto'o and Mourinho won the treble at Inter Milan in 2010
Wanaungana tena: Eto'o na Mourinho walitwaa mataji matatu Inter Milan mwaka 2010
Treble
Maswali tu ni kwamba bado ana kasi ile ile iliyomfanya tishio kwa wapinzani Italia na Hispania na kulikuwa kuna ushahidi mwaka jana katika Ligi ya Urusi na Ulaya, Europa League kwamba kasi yake inapungua sambamba na kuongezeka kwa umri wake.
Pamoja na hayo, shaka juu ya kasi yake inaondolewa na uhusiano wake na mchezaji mpya mwingine wa Chelsea kutoka Anzhi, Mbrazil Willian, ambao umekuwa ukizalisha mabao japo moja katika mechi mbuili. Ni bahati nasibu Mourinho anacheza kumsajili Eto’o.
"Kuna Jose Mourinho mmoja tu," Eto’o aliwahi kusema wakati fulani juu ya kocha wake huyo wa zamani. "Nimecheza chini ya makocha wengi wakubwa, lakini hakuna mtu mfano wa Jose katika katika mchezo huu,". 
defeat: The signing effectively kills any hope Mourinho had of signing United striker Rooney
Pio: Mourinho amemkosa mshambuliaji wa United, Rooney
Writing's on the wall: Wayne Rooney took to Facebook to thank Old Trafford fans on Monday night
Alichoandika kwenye ukurasa wake: Wayne Rooney ametumia ukurasa wake wa Facebook kuwashukuru mashabiki wa Old Trafford kwa sapoti waliyompa kwenye mechi dhidi ya Chelsea

"Ningependa kupata nafasi ya kucheza chini yake tena, kwa sababu haijawahi kuboa napokuwa karibu na Jose,".
Kutua kwa Eto’o ni kama pigo kwa washambuliaji wa tatu wa timu hiyo ya Stamford Bridge. Fernando Torres na Romelu Lukaku walikuwa benchi Old Trafford usiku wa Jumatatu na Demba Ba, anayetakiwa kurejea Newcastle na kocha Alan Pardew, hakuwamo kabisa kikosini.
Kutua kwa Willian na Eto’o haiwezi kuwa dalili za Chelsea kumaliza kununua wachezaji, kwani klabu hiyo pia ipo kwenye mazungumzo na Porto juu ya Christian Atsu, winga mwenye thamani ya Pauni Milioni 4, ambaye pia aliwahi kutakiwa na Cardiff, Tottenham na Liverpool. Na mchezaji huyo wa timu ya taifa ya Ghana chini ya umri wa miaka 21 kuna matumaini makubwa akaungana na magwiji wa Chelsea.
Lakini iwapo watafanikiwa kumsaini Atsu mbele ya Spurs walioamua kumwaga fedha sokoni, litakuwa pigo la pili kwa Andre Villas-Boas majira haya ya joto, kufuatia kuzidiwa kete kwa Willian.
All in blue: The Brazilian will wear the No 22 shirt
Wote tabasamu: Kiungo wa Brazil, Willian amefurahia kukamilisha usajili wake Stamford Bridge
Willian at Chelsea

0 comments:

NEYMAR ATWAA TAJI LA KWANZA BARCA., MESSI AREJEA UWANJANI LAKINI AKOSA PENALTI CAMP NOU

NYOTA wa Brazil, Neymar ameshinda taji lake la kwanza Barcelona kufuatia vigogo hao wa Katalunya kutwaa taji la nne la Super Cup ya Hispania ndani ya miaka mitano kwa faida ya bao la ugenini, baada ya sare bila kufungana  0-0 usiku wa jana Uwanja wa Nou Camp.
Baada ya sare ya 1-1 wiki iliyopita Uwanja wa Calderon, bao la Barca likifungwa na Neymar, aliyetokea benchi kuisawazishia timu hiyo mjini Madrid, alianzishwa katika kikosi cha kwanza kwa mara ya kwanza tangu ajiunge na timu hiyo majira haya ya joto akitokea Santos ya kwao.
Mwanasoka Bora wa Dunia, Lionel Messi pia alirejea uwanjani baada ya kuwa majeruhi, lakini wote walishindwa kutikisa nyavu za wageni.
Messi alikosa hadi penalti baada ya kugongesha mwamba na mpira ukarejea uwanjani.
Katika mchezo huo, wachezaji wawili walitolewa nje kwa kadi nyekundu, Filipe Kasmirski dakika ya 80 na Arda Turan dakika ya 90 n

0 comments:

BONDIA WA MAREKANI ATAMBA KUMSAMBARATISHA BONDIA CHEKA KESHO DIAMONDI JUBILEE

Bondia Phil Williams wa marekani akiwa na mkanda wake wa ubingwa wa WBU mara baada ya kuwasiri nchini
WAKATI bondia wa nchini Marekani, Phil Williams akipima uzito leo, amejigamba kumfanyia kitu mbaya mpinzani wake Francis Cheka. Pambano hilo la kuwania ubingwa wa Dunia, limepangwa kufanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.

Rais wa TPBO, Yassin Abdallah alisema mpinzani wa Cheka

0 comments:

''TUNATAKA SERIKALI MBILI'' WAKUU WA MKOA NA WALIYA

WAKUU wa mikoa na wilaya nchini, jana waliungana na wananchi wengine kutoa maoni kwa ajili ya kuboresha rasimu ya Katiba mpya. Katika maoni yao, viongozi hao wa mikoa na wilaya walipendekeza Katiba mpya iweke muundo wa serikali mbili kwa madai kuwa muundo huo utasaidia kulinda Muungano.

Viongozi hao walisema muundo mwingine tofauti na serikali mbili ni hatari na kwamba muundo wa serikali tatu haufai, kwani unaweka mwanya wa Muungano kuvunjika.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, mwenyekiti wa jopo hilo, ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro, alisema huo ndiyo msimamo wa baraza lao.

Kandoro alisema baraza lao limejikita zaidi kujadili masuala muhimu na kueleza kuwa wamepandekeza mambo manne kwa lengo la kuiboresha rasimu hiyo.

“Rasimu ya Katiba imetoa mfumo wake utakuwa na shirikisho linaloundwa na serikali Tatu ‘Ibara 57(1) yaani Serikali ya Jamhuri ya Muungano, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na Serikali ya Tanganyika.

“Sababu zetu za msingi kwa mgawanyiko wa nchi yetu ilivyo, kuna kila dalili ya rasilimali zinazotegemewa kuendesha kwa kiasi kikubwa serikali zote tatu zinazopendekezwa kuuweka Muungano huo katika hali tete,” alisema.

“Pia tumependekeza masuala ya kisheria, Katiba kama sheria mama iundwe kwa lengo la kutoa matamko ya msingi ya haki na wajibu wa wananchi, viongozi na

0 comments:

SUGU: SERIKALI IUNDE TUME YA KUSAIDIA WASANII WA TANZANIA

MBUNGE wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi 'Sugu', ameitaka Serikali kuunda tume huru kuchunguza mapato ya wasanii yanayoibiwa na kampuni za simu nchini,

0 comments:

ZAIDI YA MASAA MANNE YATUMIKA KUTENGANISHA MAPACHA WALIOKUWA WAMEUNGANA MUHIMBILI

 
Jopo la Madaktari Bingwa Saba wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) na Taasisi ya Mifupa ya hospitali hiyo (Moi), wamefanikiwa kuwatenganisha pacha waliokuwa wameungana kiwiliwili.
Iliwalazimu mabingwa hao kutumia saa nne kufanikisha upasuaji huo. Mmoja wa watoto hao waliotenganishwa, amelazwa kwenye Wodi ya Uangalizi Maalumu (ICU) Taasisi ya Mifupa Moi wakati kiwiliwili kingine kilifariki.
Jopo la madaktari waliofanikisha upasuaji huo ni; bingwa mstaafu wa watoto ambaye aliitwa maalumu kwa kazi hiyo, Petronila Ngiloi, Dk Robert Mhina (mifupa) na Profesa Karim Manji aliyekuwa akifuatilia kwa karibu mapigo ya moyo.
Wengine ni Dk Karima Khalid aliyekuwa akiratibu dawa ya usingizi, Dk Hamis Shaaban (ubongo na uti wa mgongo), Dk Zaitun Bokhary (bingwa upasuaji watoto) na Dk Nyangasa (moyo na mishipa ya fahamu).
Akizungumza baada ya upasuaji huo, Dk Shaaban alisema walimfanyia vipimo mtoto ambaye hakuwa amekamilika na kugundulika kuwa hakuwa amekamilika viungo vyote achilia mbali kutokuwa na kichwa na macho pia hakuwa na moyo, figo, tumbo, maini ila alikuwa na uti wa mgongo.
“Uti wa mgongo ulikuwepo na ndio uliokuwa umeshikana na mwenzake na kuna mshipa mmoja wa fahamu ulikuwa unafanya kazi ndio maana alikuwa ukimgusa anachezesha mguu.”
Alisema kinachoratibiwa kwa sasa ni kuangalia dawa ya usingizi aliyopewa mtoto ambaye anaendelea kupumua na kwamba ndani ya saa 24, dawa ya usingizi waliyomuwekea mtoto huyo itakuwa imeisha na ataanza kunyonya kama kawaida

0 comments:

KASEJA SASA KULA SHAVU NDANI YA FC LUPOPO JAMHURI YA KIDEMOCRASIA YA KONGO

DAU alilotengewa Golikipa namba moja wa timu ya Taifa, Juma Kaseja na klabu ya FC Lupopo ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ni zaidi ya ada ya uhamisho waliyotumia TP Mazembe kumsajili Mbwana Samatta, kutoka klabu ya Simba mwaka 2011, ambayo ilikuwa dola 150,000 (sawa na Sh milioni 225).

Akizungumza na MTANZANIA jana jijini Dar es Salaam, Meneja wa Lupopo Balanga Ismael alisema, Kaseja, atajiunga rasmi na FC Lupopo, mara baada ya kumaliza

0 comments:

HAKIKA TUSIPOKUA MAKINI TOFAUTI ZETU ZITATUMALIZA EAC

 
Sasa ni bayana kwamba tofauti zilizopo miongoni mwa baadhi ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), zimeanza kukuzwa, huku wachambuzi wa masuala ya kidiplomasia wakionya kwamba tofauti hizo zisipotatuliwa haraka jumuiya hiyo itasambaratika na kubaki historia.
Sote tunatambua kwamba tofauti hizo zilianza baada ya Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania kumshauri Rais Paul Kagame kuzungumza na FDLR ambao

0 comments:

MWANAJESHI WA TANZANIA AUAWA NA WAASI WA 23 NCHINI CONGO

 
Mashirika. Mpiganaji wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania, JWTZ Khatibu Mshindo aliuawa kwa kupigwa bomu juzi na waasi wa M23 kwenye Mji wa Goma ulioko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo baada ya kuzuka mapigano makali.
Wakati Mshindo ambaye alikuwa miongoni mwa askari wa Tanzania wanaounda Jeshi la Umoja wa Mataifa akifikwa na mauti, wapiganaji wengine 10 walijeruhiwa.
Askari wa Tanzania na wale wa Afrika Kusini wako DRC kwa kazi ya kulinda amani. Malawi bado haijapeleka majeshi yake.Hali si ya utulivu huko Goma
Meja Mshindo alikuwemo katika kikosi cha vifaru na alikuwa kwenye Kambi ya 83KJ iliyoko Kiluvya Dar es Salaam.
Kuuawa kwa askari huyo kumekuja ikiwa ni siku 47 tangu kuuawa kwa askari saba wa Tanzania waliokuwa wakilinda amani kwenye Mji wa Darfur Sudan na Kikundi cha Janjaweed.
Msemaji wa JWTZ, Meja Erick Komba alikiri kutokea kifo hicho na kusema: “Jana (juzi) Agosti 28, Wanajeshi wetu wakiwa katika eneo lao la ulinzi

0 comments:

BINGWA WA DUNIA WA NDONDI MAREKANI ATUA DAR KUMKABILI CHEKA IJUMAA HII

Kocha wa mchezo wa masumbwi nchini Rajabu Mhamila 'Super D' kulia akiwa na bondia Phil Williams wa marekani baada ya kutua nchini kwa ajili ya mpambano wake na Francis Cheka utakaofanyika August 30 siku ya ijumaa hii  katika ukumbi wa Diamon Jubilee jijini Dar es salaam Picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Bondia Phil Williams wa marekani akiwa katika picha ya pamoja na wadau wa mchezo huo kushoto ni promota Jay Msangi kulia ni Kocha wa kimataifa wa mchezo wa ngumi Rajabu Mhamila 'Super D wengine ni wadau waliokuja kulaki uwanja wa ndege baada ya kutua usiku huu picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com
Mdau wa michezo nchini Saidi kindeka kushoto akiwa na Bondia Phil Williams wa marekani
Bondia Phil Williams wa marekani akiwa katika picha ya pamoja na wadau wa mchezo huo kushoto ni promota Jay Msangi kulia ni Kocha wa kimataifa wa mchezo wa ngumi Rajabu Mhamila 'Super D wengine ni wadau waliokuja kulaki uwanja wa ndege baada ya kutua usiku huu picha na www.superdboxingcoach.blogspot.com

Bondia Phil Williams wa marekani akiwa na mkanda wake wa ubingwa wa WBU
Bondia Phil Williams wa marekani akiwa na mkanda wake wa ubingwa wa WBU
Bondia Phil Williams wa marekani

0 comments: