Ni nadra kwa wanaume kukubali kufunga uzazi, lakini waliofanya hivyo wameona mafanikio yake.
Sumbawanga. “Baada ya kupata
mtoto wa nne nilidhani mke wangu asingeweza tena kushika mimba kutokana
na umri aliokuwa nao, lakini nilishangaa baada ya kukaa miaka kumi
akapata ujauzito na ndipo nilipoamua kwenda kufunga uzazi,”anasema Bevin
Mtendo (55).
Mtendo, ambaye ni Mkuu wa Idara ya Usafi wa
Mazingira Wilaya ya Sumbawanga Mkoa wa Rukwa amekuwa kivutio kikubwa
kwenye jamii tangu alipoamua kufunga uzazi mwaka 2008 kutokana na
wanaume wengi kumfuata kuomba ushauri.
Anasema ana watoto watano na kwamba mtoto wa
mwisho alimpata baada ya miaka kumi baada ya kudhani kuwa mke wake
asingeweza kuzaa tena.
Anasema kabla ya kufunga uzazi, mke wake alikuwa
akitumia njia za kisasa za uzazi wa mpango, lakini baada ya kujifungua
mtoto wa nne aliacha na kudhani kuwa hawezi kupata tena ujauzito.
Hata hivyo, anasema baada ya miaka kumi kupita mkewe alipata ujauzito hali iliyomlazimu yeye kuamua afunge uzazi.
“Tulijua hatuwezi kupata tena mtoto, lakini
alipokuja huyu wa tano
niliona sasa bora mimi nikafunge na nilipomwambia mke wangu alifurahi,”anasema.
niliona sasa bora mimi nikafunge na nilipomwambia mke wangu alifurahi,”anasema.
Mtendo anasema alishauriwa na rafiki yake ambaye naye alifunga baada ya kupata watoto wanane.
“Mwanzoni watu wengi walinishangaa na kudhani
siwezi kufurahia tena tendo la ndoa, lakini siyo kweli nafurahia vizuri
tena situmii muda mrefu na nikihitaji huduma hiyo napewa,”anasema na
kuongeza:
“Kama unahisi umepata watoto wa kutosha, njia nzuri ni kufunga na kama unataka kuamini gonga gogo usikie mlio wake,”anasema.
Kwa kawaida operesheni ndogo kwa ajili ya kufunga
uzazi huchukua kati ya dakika 15 hadi 20, lakini Mtendo anasema kwake
yeye ilimchukua dakika 45 kwa sababu aliyemfanyia alikuwa hajatoa huduma
hiyo kwa muda mrefu.
Kuhusu dhana kwamba mwanamume aliyefunga uzazi
anakuwa siyo rijali tena, Mtendo anajibu: “Siyo kweli kabisa tena
urijali unaongezeka na hata mke wangu sasa hivi anafurahi zaidi kwa
sababu awali kabla sijafanyiwa nilikuwa natumia muda mfupi, lakini sasa
hivi natumia muda mrefu kidogo na kuna siku huwa namshinda.”
0 comments: