HATA
hivyo pambano hilo pamoja na yale ya utangulizi yaliingia dosari baada
ya wachezaji kama Alfonce Mchumiatumbo, aliyekuwa akizichapa na Chupac
Chipindi katika pambano lao la utangulizi la raundi sita, kugoma kupanda
ulingoni kwa kile walichokuwa wakieleza mabondia hao kuwa wanahitaji
kumaliziwa pesa zao za mkataba wa kucheza mechi hizo kabla ya kupanda
ulingoni.
Nao
mabondia Mada Maugo na Thomas Mashali, pia waligoma kupanda ulingoni
wakishinikiza kumaliziwa pesa zao kwanza jambo ambalo lilifanya kuzua
taflani ukumbini hapoa huku mapambano yakichelewa kuanza.
Ilipofika
muda wa Cheka kupanda ulingoni pia alisikika mtangazaji akimuita
muandaaji wa mapambano hayo ili kufika chumba alichokuwa Bondia
mtanzania, Francis Cheka ili kumalizana naye mkwanja ili akubali kupanda
ulingoni.
Alisikika
Cheka akimuwakia muandaaji huyo kuwa, '' Nini Mmarekani hata angekuwa
Mchina, nimalizie changu kwanza ili nipande ulingoni, ambalo pia
lilichukua muda wa majadiliano hadi kuingiliwa kati na wadhamini na
wadau wa ngumi waliotangaza kujikomiti kulipa pesa hizo wanazodai
mabondia, ndipo mabondia hapo wakapanda ulingoni.
Aidha
katika pambano la raundi 10 la mabondia Mada Maugo na Thomas Mashali la
kuwania Ubingwa wa WBF wa Afrika, Thomas Mashali ameweza kumshinda kwa
pointi 2 tu mpinzani wake Mada Maugo na kutwaa Mkanda huo wa ubingwa wa
WBF wa Afrika.
Na
katika pambano la Utito wa Juu la utangulizi la Raundi sita kati ya
Bondia Alfonce Mchumiatumbo na Chupac Chipindi, Mchumiatumbo amemchapa
kwa KO mpinzani wake katika raundi ya tano, baada Chupac kunyoosha
mikono juu kuashiria na wasaidizi wake kutupa taulo ulingoni kuashiria
kushindwa kumalizia mchezo huo.
0 comments: