Hali ya usalama kwenye Kituo Kikuu cha Mabasi yaendayo Mikoani (UBT), imekuwa tete baada ya kuibuka kwa kundi kubwa la matapeli wanaowaibia abiria na kuwabambikizia kesi kwa kutumia njia ya ulinzi shirikishi.
Mbali na kufanyika kwa vitendo hivyo kituo hicho
kinadaiwa kuwa soko kubwa la biashara haramu ya dawa za kulevya aina ya
Bangi na Mirungi.
Kundi hilo ambalo linajulikana kama vishoka
limekuwa likifanya vitendo hivyo kuanzia saa mbili usiku kwa kujifanya
kuwa wao ulinzi shirikishi, na kufanya utapeli huo kwa kuwakamata abiria
na baadhi ya watu wanaoingia kwenye kituo hicho na kuwapa makosa
mbalimbali.
Uchunguzi uliyofanywa na gazeti hili takriban siku
tatu kwenye kituo hicho majira usiku na mchana, umebaini kwamba mchezo
huo mchafu umekuwa ukifanyika kwa muda mrefu ambapo tayari kundi kubwa
la watu wametapeliwa na kuibiwa vitu mbalimbali.
Uchunguzi huo umebaini kwamba moja ya utapeli
unaofanywa na kundi hilo la vijana wanaojiita ulinzi shirikishi, ni
kutumia pete feki za dhahabu ambazo wanazitumia kuwatapeli fedha abiria.
Pia, licha ya kufanya utapeli huo kwa kutumia
dhahabu feki, kundi hilo linatumia bidhaa ya sabuni kuwatapeli simu
abiria. Sabuni hutengenezwa kwa mfano wa simu na kuwabambika watu kuwa
ni simu halisi.
Licha ya kufanyika kwa vitendo hivyo, uchunguzi
pia umebaini kuwepo
kwa biashara haramu ya dawa za kulevya aina ya bangi na mirungi.
kwa biashara haramu ya dawa za kulevya aina ya bangi na mirungi.
Uchunguzi pia umebaini kwamba vijana hao matapeli
wakimkamata mtu kwa kisingizio cha kuhusika na wizi, wanamtoza faini
kati ya Sh50,000 hadi 70,000. Makosa yanayodaiwa kuwa madogo kama
kukojoa au kutupa uchafu wanatoza faini ya kati ya Sh10,000 hadi
Sh20,000 kila siku.
Akizungumzia suala hilo Mwenyekiti wa Serikali ya
Mtaa wa Ubungo (NHC), Amani Sizia alithibitisha kuwepo kwa vitendo hivyo
vya uhalifu na kudai kwamba UBT imegeuka kuwa shamba la bibi kwa
wahalifu.
Sizia alisema: “Kwa kweli hali ya kituo cha mabasi
ya Ubungo na maeneo jirani imekuwa mbaya sana, kuna vikundi vya ulinzi
shirikishi ambavyo ni feki zaidi ya vitano. Vikundi hivyo vimekuwa
vikifanya kazi ya kuwatapeli abiria.”
Alisema kwa kuthibitisha zaidi nyakati za usiku
kila kibaka anageuka kuwa mlinzi shirikishi, na kufanya kazi ya utapeli
ili kujipatia fedha.
“Nashukuru sana ndugu yangu mwandishi kwa
kunitafuta UBT kwa sasa haifai, kuna vitendo vingi vya uhalifu ambavyo
vinafanyika nyakati za usiku. Kila kibaka ikifika wakati huo anageuka
kuwa mlinzi shirikishi,” alisema Sizia
0 comments: