MAFUNDISHO YA MUNGU NA MTUMISHI WA MUNGU JOSEPHAT .E. MWINGIRA



DARASA/CHUMBA CHA MAFUNDISHO: ''Mkalimani Mtumishi wa MUNGU Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, Efatha Ministry.
(Darasa linaendelea lilipoishia....)

"Katika kila msuguano kuna kisababisho ambacho kina mzizi na huo mzizi ukijulikana utang’olewa na uking’olewa ndipo kipindi cha burudiko kitakujulia. Kipindi hiki kitakujilia pale tu huo mzizi utakuwa umeondolewa.

Zaburi 139: 23 -24 “Ee MUNGU unichunguze uujue moyo wangu, unijaribu uyajue mawazo yangu, uone kama iko njia iletayo majuto ndani yangu; ukaniongoze katika njia ya milele”, HAYA NDIO MAOMBI ya mtu anayetaka kupona na kufunguliwa katika vifungo vilivyopo ndani yake; anayetafuta WEMA WA BWANA utokee kwake; ANAYETESEKA anatafuta kiini cha mateso yake; aliye na taabu anayemlilia BWANA apate kumjulisha kiini cha tabu yake; mama aliye na TATIZO la NDOA anayemlilia BWANA apate kumkumbuka."

(USIKOSE Darasa ni NEEMA yako hii ya USHINDI, YESU Anakupenda)
Share on Google Plus

0 comments: