NI NAFASI YAKO YA KUSOMA BARUA HII YA MCHEZAJI KAZI MOTO KWA WATANZANIA WOTE NA TFF AKIOMBA MSAMAHA...


AL MARKHIYA SPORTS CLUB
P O BOX 21923
DOHA, QATAR
TANZANIA FOOTBALL FEDERATION
P O BOX 1574
DAR-ES-SALAAM 
TANZANIA

YAH: KUOMBA MSAMAHA KWA CHAMA CHA MPIRA TANZANIA
Husika na kichwa cha habari hapo juu mimi mchezaji MWINYI KAZIMOTO naomba msamaha kwa kitendo nilichokifanya cha kuondoka kambini timu ya taifa na kuiacha nchi yangu katika kipindi kigumu hali ya kuwa walikuwa na mechi ngumu na muhimu dhidi ya Uganda.
Halikuwa lengo langu kuidhoofisha nchi yangu bali ni tamaa yangu ya kucheza mpira nje ya nchi ndiyo iliyonifanya niondoke katika kipindi hicho, na nashukuru mungu nimefanikiwa kupata team nchini Qatar, naamini watanzania wataipokea habari hii kwa vizuri.
Mwisho kabisa napenda kuwahakikishia watanzania na chama cha mpira kwa ujumla kwamba naahidi nitaitumikia nchi yangu muda wowote watakaponihitaji.
Natumai chama cha mpira na watanzania kwa ujumla watanielewa na watanisamehe.
Wenu mtiifu

MWINYI KAZIMOTO
Share on Google Plus

0 comments: