Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania
Bara msimu wa 2013/2014 inaanza kutimua vumbi Agosti 24 mwaka huu kwa timu zote
14 kuwa viwanjani katika miji saba tofauti.
Hata hivyo, kabla ya ligi hiyo kuanza kutakuwa na mechi
ya kufungua msimu (Ngao ya Jamii- Community Shield) kati ya bingwa mtetezi Yanga
na Makamu bingwa Azam itakayochezwa Agosti 17 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es
Salaam.
Mechi za VPL za Agosti 14 mwaka huu zitakuwa kati ya
Yanga na Ashanti United (Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam), Mtibwa Sugar na Azam
(Uwanja wa Manungu, Morogoro), na JKT Oljoro na Coastal Union (Uwanja wa
Kumbukumbu ya Sheikh Kaluta Amri Abeid, Arusha).
Nyingine ni Mgambo Shooting na JKT Ruvu (Uwanja wa
Mkwakwani, Tanga), Rhino Rangers na Simba (Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, Tabora),
Mbeya City na Kagera Sugar (Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine, Mbeya), na Ruvu
Shooting na Tanzania Prisons (Uwanja wa Mabatini, Mlandizi,
Pwani).
Mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo utamalizika Novemba 3
mwaka huu wakati wa pili utamalizika Aprili 27
mwakani.
TAIFA STARS KWENDA KAMPALA
J5
Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inaondoka
Mwanza keshokutwa (Julai 24 mwaka huu) kwenda Kampala, Uganda kwa ajili ya mechi
ya marudiano ya Kombe la CHAN itakayochezwa Jumamosi (Julai 27 mwaka huu) Uwanja
wa Mandela kuanzia saa 10 kamili jioni.
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager
iko kambini jijini Mwanza chini ya Kocha Kim Poulsen tangu Julai 14 mwaka huu
kujiandaa kwa mechi hiyo itakayoamua ni timu ipi kati ya hizo mbili itacheza
Fainali za CHAN zitakazofanyika mwakani nchini Afrika
Kusini.
Timu hiyo itaondoka Uwanja wa Ndege wa Mwanza saa 7.25
mchana kwa ndege ya PrecisionAir, na inatarajiwa kutua Uwanja wa Ndege wa
Kimataifa wa Entebbe saa 10.15 jioni.
Wakati huo huo, Kocha Kim Poulsen kesho (Julai 23 mwaka
huu) atakuwa na mkutano na waandishi wa habari kuzungumzia maandalizi ya kikosi
chake. Mkutano huo utafanyika saa 5 kamili asubuhi kwenye hoteli ya La Kairo
jijini Mwanza.
WAAMUZI WA MCHEZO WA STARS VS UGANDA
Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limeteua
waamuzi kutoka Madagascar kuchezesha mechi kati ya Tanzania (Taifa Stars) na
Uganda (The Cranes) itakayochezwa Jumamosi (Julai 27 mwaka huu) Uwanja wa
Mandela ulioko Namboole nje kidogo ya Jiji la
Kampala.
Waamuzi wataongozwa na Kanoso Abdoul Ohabee wakati
mwamuzi msaidizi namba moja ni Andirvoavonjy Pierre Jean Eric. Mwamuzi msaidizi
namba mbili ni Jinoro Velomanana Ferdinand huku Andriamiharisoa Hubert Marie
Bruno akiwa mwamuzi wa mezani (fourth official).
Kamishna wa mechi hiyo ya marudiano ya raundi ya mwisho
kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) ni
Ismail Kamal kutoka Ethiopia.
Mechi hiyo namba 38 itachezwa kuanzia saa 10 kamili
jioni kwa saa za Afrika Mashariki. Taifa Stars ilipoteza mechi ya kwanza
iliyochezwa Julai 13 mwaka huu jijini Dar es Salaam kwa bao
1-0.
Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager
iko kambini jijini Mwanza ikijiandaa kwa mechi hiyo itakayoamua ni timu ipi kati
ya hizo mbili itacheza Fainali za CHAN mwakani nchini Afrika
Kusini.
0 comments: