
Ni wiki ya pili sasa tangu Afrika Kusini ikumbwe na vurugu zinazoambatana na mauaji zinazosababishwa na makundi ya watu wenye silaha ambayo yanawalaumu wahamiaji wa Kiafrika kwa kuchukua kazi zao.
Nhlanhla amelaani mauaji hayo na kupitia akaunti yake ya Instagram hivi karibuni amewaomba mashabiki wake, marafiki na wengine wote kuungana katika kuwasaidia wahanga wa vurugu hizo zinazoendelea.
Rais nchi hiyo, Jacob Zuma amesitisha ziara yake ya nchini Indonesia ili kukabiliana na vurugu hizo huku akiwatembelea watu walioathirika.

Vurugu zikiendelea katika Mji wa Durban, Afrika Kusini.
0 comments: