Mjumbe wa Bunge la Katiba Kangi Lugola, ametaja msimamo wake wa kuunga mkono serikali tatu kwamba ni kukwepa unafiki.
Lugola, ambaye alisema kwenye kikao cha Bunge la
Katiba kuwa atakuwa wa mwisho kuisaliti Rasimu ya Tume ya Mabadiliko ya
Katiba, alisema kinachowasumbua wanasiasa wengi ni suala la unafiki
ambalo ameapa hatakuwa tayari kulisujudia.
Akizungumza na gazeti hili kuhusu msimamo wake
unaopingana na chama chake cha CCM, alisema wanaounga mkono miongozo ya
vyama kwenye Bunge la Katiba, wanafanya hivyo kwa unafiki na hofu ya
kisiasa.
Alisema kitendo cha kupinga Rasimu ya Pili ya
Katiba ambayo iliwasilishwa na mwenyekiti wa Tume, Jaji Joseph Warioba,
ni sawa na kupinga mawazo ya wananchi.
“Tumetumia fedha nyingi kwa ajili ya Tume ya Jaji
Warioba kukusanya maoni ya wananchi na alichokileta bungeni ni matakwa
ya Watanzania. Leo hii tunaanza kuchakachua kile ambacho alikifanyia
kazi kwa uaminifu mkubwa?” alihoji Lugola.
Alisema hawezi kukubaliana na dhambi ya unafiki. “Nawataka wana-CCM wenzangu muweze kupima mambo badala ya kuburutwa,” alisema.
Kuhusu muundo wa Muungano, alisema hata sasa hakuna Muungano kwani Zanzibar imeshajitangazia mamlaka yake.
“Kama wanataka kurudisha Muungano, Serikali ya
Zanzibar inatakiwa ivunjwe ili ieleweke kuwa hakuna Tanganyika na hakuna
Zanzibar. Sasa hakuna lolote ambalo linaweza kunishawishi kuwa kuna
Muungano,” alisema Lugola.
“Muundo wa be huyo alisema kuwa serikali tatu
unawezekana na tayari upo unafanya kazi, lakini ukiwa katika kivuli cha
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,” alisema ambaye wiki iliyopita
aliwatahadharisha wajumbe wenzake dhidi ya hatari kwa wengi kuwaburuza
wachache.
0 comments: