WANAOKUBALI SERIKALI TATU WANAKWEPA UNAFIKI, KANGI LUGOLA



Mjumbe wa Bunge la Katiba Kangi Lugola, ametaja msimamo wake wa kuunga mkono serikali tatu kwamba ni kukwepa unafiki.
Lugola, ambaye alisema kwenye kikao cha Bunge la Katiba kuwa atakuwa wa mwisho kuisaliti Rasimu ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba, alisema kinachowasumbua wanasiasa wengi ni suala la unafiki ambalo ameapa hatakuwa tayari kulisujudia.
Akizungumza na gazeti hili kuhusu msimamo wake unaopingana na chama chake cha CCM, alisema wanaounga mkono miongozo ya vyama kwenye Bunge la Katiba, wanafanya hivyo kwa unafiki na hofu ya kisiasa.
 Alisema kitendo cha kupinga Rasimu ya Pili ya Katiba ambayo iliwasilishwa na  mwenyekiti wa Tume, Jaji Joseph Warioba, ni sawa na kupinga mawazo ya wananchi.
“Tumetumia fedha nyingi kwa ajili ya Tume ya Jaji Warioba kukusanya maoni ya wananchi na alichokileta bungeni ni matakwa ya Watanzania. Leo hii tunaanza kuchakachua kile ambacho alikifanyia kazi kwa uaminifu mkubwa?” alihoji Lugola.
Alisema hawezi kukubaliana na dhambi ya unafiki. “Nawataka wana-CCM wenzangu muweze kupima mambo badala ya kuburutwa,” alisema.
Kuhusu muundo wa Muungano, alisema hata sasa hakuna Muungano kwani Zanzibar imeshajitangazia mamlaka yake.
“Kama wanataka kurudisha Muungano, Serikali ya Zanzibar inatakiwa ivunjwe ili ieleweke kuwa hakuna Tanganyika na hakuna Zanzibar. Sasa hakuna lolote ambalo linaweza kunishawishi kuwa kuna Muungano,” alisema Lugola.
“Muundo wa be huyo alisema kuwa serikali tatu unawezekana na tayari upo unafanya kazi, lakini ukiwa katika kivuli cha Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,” alisema ambaye wiki iliyopita aliwatahadharisha wajumbe wenzake dhidi ya hatari kwa wengi kuwaburuza wachache.
Share on Google Plus

0 comments: