Msemaji
 Mkuu wa Wizara ya Fedha, Ingiahedi Mduma, akizungumza wakati wa Semina 
maalum kwa 'Mablogger', iliyofanyika katika Hoteli ya Kilimanjaro Park, 
Misugusugu Kibaha, hivi karibuni. Semina hiyo imeandaliwa na Wizara ya 
Fedha kwa lengo la utaratibu wa kutimiza utekelezaji wa Matokeo Makubwa 
Sasa (Big Results Now). Picha na Sufianimafoto.com
******************************
 Na Mwandishi Wetu
Serikali
 inalenga kushirikiana na sekta binafsi katika kutekeleza miradi ya 
kimkakati yenye thamani ya shilingi trioni 6 hadi kufikia mwaka 2015/16 
ikiwa ni sehemu ya ukamilishwaji wa mkakati wa “Tekeleza kwa Matokeo 
Makubwa Sasa” yaani Big Results Now (BRN), utaratibu unaotumiwa na 
Serikali katika kusimamia na kufuatilia utekelezaji wa baadhi ya 
majukumu yake kwa lengo la kupata matokeo makubwa kwa muda mfupi. 
Katika
 mkuitano wake na wamiliki wa magazeti tando, msemaji mkuu wa wizara ya 
Fedha, Bi Ingiahedi Mduma alibainisha kuwa kuna vyanzo vingi vya fedha 
ambavyo wizara yake imedhamiria kuvitumia lakini kwa hii ambayo 
wanatarajia kushirikisha sekta binafsi ipo miradi mitatu mikuu ambayo 
inatarajiwa kutoa muongozo.

Bi
 mduma aliitaja miradi hiyo ya awali kuanza kutekelezwa kwa ubia ni 
ujenzi wa barabara ya Dar es Salaam hadi Chalinze, uendeshaji wa Mradi 
wa Mabasi yaendayo haraka jijini Dar es Salaam, na ujenzi wa kituo cha 
kufua umeme cha Kinyerezi III. 
Amesema
 ukiachana na miradi hii, Wizara ya Fedha inaendelea kutekeleza jukumu 
la kutafuta na kutoa fedha za kugharamia shughuli za BRN zilizoibuliwa 
katika maabara zote sita za Elimu, Maji, Kilimo, Uchukuzi, Nishati na 
utafutaji na mapato ya serikali.
Bi
 Mduma ameelezea pia kwamba katika kipindi cha Julai hadi Disemba, 2013 
Wizara ya Fedha imefanikiwa kutekeleza kiashiria hiki kwa kutoa fedha za
 maendeleo za ndani kwenye Wizara zinazotekeleza shughuli za BRN.
Amesema
 jumla ya shilingi Bilioni 590.5 zimetolewa katika kuhakikisha kwamba 
maabara hizi zinaweza kujitegemea katika miradi yake.
Akitaja
 viwango nvya fedha ambavyo wizara imetoa, Bi Mduma alisema miradi ya 
Elimu imepewa jumla ya shilingi bilioni 8.3, Miradi ya Maji imepewa 
shilingi bilioni 86.0, Miradi ya Kilimo shilingi bilioni 10.2, Miradi ya
 Uchukuzi shilingi bilioni 146.6 na Miradi ya Nishati imepewa jumla ya 
shilingi bilioni 339.4.


0 comments: