DARASA/KONA YA MAFUNDISHO: ''Mkalimani Mtumishi wa MUNGU Mtume na Nabii Josephat

Photo: Naibariki Jumamosi yangu... (Darasa linaendelea lilipoishia jana,... Pata UFAHAMU ili UWE HURU na MSHINDI).
Tatizo ambalo MUNGU Aliruhusu mwenyewe ni:- .
Ahabu alipotakiwa afe kwa sababu njia zake hazikumpendeza MUNGU, MUNGU Aliitisha kikao, MUNGU Akasababisha laana itokee hata kwa wale makuhani. Akauliza nani anaweza kumdanganya Ahabu ili akafe, vita ikaanzishwa ambayo haikuwepo ili tu Ahabu akafe.

N.B. Siyo kila vita inayoanzishwa unaruhusiwa uende ukapigane, tambua imetoka wapi kwanza. Ahabu alijiandaa kwenda kupigana, manabii wakaja na shetani naye akajitokeza kwa MUNGU.
(Kwa kutaka kuijua zaidi habari hii soma 1Falme 22:)

MUNGU Anapoamua kuleta mabaya mahali anamruhusu shetani mzoefu wa maovu. Kama MUNGU Akiona njia zako hazijanyooka na unapoelekezwa hutaki kuelewa, una masikio ya utafiti; MUNGU Anairuhusu roho ya upotevu ikufuate. Manabii wa uongo wanajitokeza.

(Darasa litaendelea wiki ijayo, USIKOSE Mwana wa MUNGU Wewe uliyedhamiria kuwa HURU, kuwa HURU KWELI KWELI, Ubarikiwe.)
(Darasa linaendelea lilipoishia jana,... Pata UFAHAMU ili UWE HURU na MSHINDI).
Share on Google Plus

0 comments: