JESHI LA KONGO LASHAMBULIA WAASI MASHARKI MWA MJI WA GOMA

 A Congolese army soldier walks through the bush, back from an attack position north-west of Munigi, overlooking the front-line, in the east of the Democratic Republic of the Congo on July 15, 2013. Fighting broke out yesterday between M23 rebels and the national army, and continued today, with heavy artillery fire north-west of Munigi and the army claiming to have taken ground. AFP PHOTO/PHIL MOORE (Photo credit should read PHIL MOORE/AFP/Getty Images)
Majeshi ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo kwa kutumia helikopta yameyashambulia maeneo ya waasi karibu na upande wa mashariki mwa mji wa Goma, ikiwa siku ya tatu ya mapigano makali yaliyosabaisha wimbi la ukimbizi.
Katika barua ilitumwa kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ambayo Shirila la habari la Reuters limepata nakala yake, Kongo imekituhumu kikosi maalumu cha
Rwanda kwa kuwasaidia waasi wa M23 katika mapigano hayo. Lakini pia katika taarifa yao walinzi wa amani wa Umoja wa Mataifa nchini Kongo wamekanusha madai ya Rwanda kwamba walifyatua makombora dhidi ya nchi hiyo kutoka ardhi ya Kongo Jumatatu.
Taarifa ya jeshi hilo la ulinzi wa amani lijulikalo kama MONUSCO, umesema wanajeshi wake hawajahusika na mapigano katika eneo la Goma na kwa hivyo hawawezi kuhusika katika kufyatua makombora kwenye mipaka ya Rwanda.CHANZO DW
Share on Google Plus

0 comments: