GAY NA POWELL KUTOSHIRIKI MASHINDANO YA DUNIA MOSCOW

 epa03775607 Tyson Gay from the USA celebrates after winning the mens 100 m race at the Athletissima IAAF Diamond League athletics meeting in the Stade Olympique de la Pontaise in Lausanne, Switzerland, 04 July 2013. EPA/JEAN-CHRISTOPHE BOTT +++(c) dpa - Bildfunk+++
Shirikisho la mchezo wa riadha duniani lasema mfumo wake wa kupambana na wanariadha wanaotumia madawa ya kuongeza nguvu unafanyakazi, wakimbiaji mashuhuri Tyson Gay na Asafa Powell wanasa katika mtego,wa Doping.
Shirikisho la mchezo wa riadha ulimwenguni IAAF limesema kuwa kuaminika kwa mpango wake wa kupambana na wanariadha wanatumia madawa ya kutunisha misuli kumeimarika na sio kuporomoka baada ya wakimbiaji nyota Asafa Powell na Tyson Gay wa Marekani kunasa katika mtego huo baada ya kupatikana na hatia ya kutumia madawa ya kuongeza nguvu, ambayo yamepigwa marufuku.
Gay , bingwa wa zamani wa dunia ambaye alishinda mbio za mita 100, na 200 katika mashindano ya kitaifa nchini Marekani mwezi uliopita, amesema kuwa atajitoa katika mashindano yajayo ya ubingwa wa dunia nchini Urusi mwezi ujao.
(FILE) A file picture dated 30 August 2007 shows Tyson Gay of the USA celebrating after winning the 200m final at the 11th IAAF World Championships in Athletics, Osaka, Japan. Tyson is awarded the 2007 Male World Athlete of the Year during the celebrations of the World Athletics Gala hosted by International Athletic Foundation (IAF) Honorary President HSH Prince Albert II of Monaco and IAF & IAAF President Lamine Diack in the Salle des Etoiles of the Sporting Club dÒEt- Monte Carlo, 25 November 2007. EPA/KIMIMASA MAYAMA +++(c) dpa - Bildfunk+++
Bingwa wa zamani wa mbio za mita 100 na 200 duniani Tyson Gay
Wakabiliwa na adhabu
Powell ambaye alishikilia rekodi ya dunia katika mbio za mita 100 hadi Usain Bolt alipoishusha mwaka 2008, pamoja na bingwa wa medali ya dhahabu katika mashindano ya Olimpiki Sherone Simpson pia wanakabiliwa ya hatua ya kuzuiwa kushiriki michezo ya riadha baada ya
kupatikana na hatia ya kutumia madawa hayo katika michezo ya chama cha riadha cha Jamaica mwezi uliopita.
FILE - In this Saturday, May 19, 2013 file photo, Asafa Powell of Jamaica, center, competes with Nesta Carter of Jamaica, left, and Kim Collins of Saint Kitts, right, during the men's 100 meter at the Diamond League track and field competition in Shanghai, China. Former 100-meter world-record holder Asafa Powell and Jamaican teammate Sherone Simpson have each tested positive for banned stimulants, according to their agent. Paul Doyle told The Associated Press on Sunday, July 14, 2013 that they tested positive for the stimulant oxilofrine at the Jamaican championships and were just recently notified. The news came the same day that American 100-meter record holder Tyson Gay revealed that he also failed a drug test. (AP Photo/Eugene Hoshiko, File)
Asafa Powell (kulia) akiwa na Nesta Carter
Msemaji wa shirikisho la michezo ya riadha duniani IAAF Nick Davies amesema shirikisho hilo haliwezi kuzungumzia kuhusu kesi ambazo bado hazijaamuliwa , lakini ameongeza kuwa mapambano dhidi ya doping yameimarishwa , na sio kuporomoka , kila mara inapowezekana kufichua kesi mpya.
Wanariadha watano ikiwa ni pamoja na washindi wawili wa medali za olimpiki walipatikana na hatia ya kutumia madawa ya kutunisha misuli katika mashindano ya riadha nchini Jamaica .CHANZO DW
Share on Google Plus

0 comments: