HII NDIO TOP FIVE (5) YA USAJIRI BORA ULIOFANYIKA NYAKATI TOFAUTITOFAUTI WENYE HISTORIA YA AJABU

1) Jose Mourinho, OK, Special One hakusajiliwa kwa namna ya kawaida kama wachezaji na alimgharimu Roman kiasi kidogo tofauti na wachezaji wengi waliomfuatia kuja Stamford Bridge, lakini Chelsea isingekuwa hivi ilivyo bila Mourinho.

Jose Mourinho remains Chelsea's most successful manager
 
Akiwa ametoka kushinda ubingwa wa champions league na FC Porto kwenye msimu wake wa mwisho na klabu hiyo ya kwao Ureno, Mourinho alichukua nafasi ya Claudio Ranieri mwezi June 2004 na kushinda ubingwa ligi na Premier League  katika msimu wake wa kwanza ndani ya Stamford Brifge.
The Blues walifanikiwa kuutetea ubingwa wao msimu uliofuata na mreno huyo akaiongoza timu hiyo kushinda League Cup na FA Cup bkabla ya kuondoka September 2007 kwa makubaliano na Chelsea.

Mapema mwezi uliopita Jose Mourinho alirudi rasmi kuifundisha Chelsea akitokea Real Madrid.

2) Didier Drogba

Alisajiliwa na Chelsea July 2004 kwa ada ya uhamisho wa £24m, Drogba alichukua muda kidogo kuanza kufunga pamoja na kufunga goli lake la kwanza katika mechi ya 3 ya kimashindano kwenye mechi dhidi ya Crystal Palace.
Mwanzoni, wachambuzi wa soka hasa wale wapenzi wa Chelsea hawakuwa wakimpa nafasi ya kufanya vizuri darajani, lakini Muafrika magharibi huyo baadae aliwaonyesha vitu vya hatari mpaka wakaanza kumtukuza kuliko baadhi ya wachezaji wengi wa timu hiyo. 

Mshambuliaji alithibitisha ukali wake kwa kuwa mmoja wa wachezaji wa kuogopwa hasa kwenye mechi kubwa. 
Akiwa ameshashinda makombe matatu ya Premier League, manne ya FA Cup, mawili yaLeague Cup ana ngao za hisani mbili, Drogba akajihakikishia nafasi katika historia ya Chelsea kwa kufunga bao la kusawazisha kwenye fainali ya UCL dhidi ya Bayern Munich kabla ya kufunga penati ya ushindi na kuipa ubingwa wa kwanza wa ulaya Chelsea. 

Didier Drogba ensured Chelsea became kings of Europe
 3) Claude Makelele, Wakati Makelele alipowasili darajani  2003, Ranieri alisema: “Nina saa nzuri sana, inaendeshwa na batri nzuri mno na Claude ndio betri yangu mpya. Claude ni muhimu sana kwa Chelsea.”
Kwa wakati huo watu wengi walimcheka juu ya maoni yako hayo lakini Makelele akawathibitishia watu hao mneno ya Ranieri kuhusu yeye.
Mfaransa huyu aliifanya Chelsea kuwa na safu ya ulinzi imara kuliko - na akazidi kuimarika pale alipokuja Mourinho darajani.
Mpaka wakati anaondoka Chelsea kwenda Paris Saint-Germain mwaka 2008, Makelele alishashinda makombe mawili ya premier league, moja la FA CUP, mawili ya ligi na moja la ngao ya hisani.
Katika kuonyesha ni namna gani aliweza kuilinda safu ya ulinzi ya Chelsea na hakuwa mtu anayependa kuacha majukumu yake na kwenda kushambulia - Makelele aliweza kufunga mabao mawili tu mpaka anaondoka kwenye klabu hiyo.
Claude Makelele made Chelsea tick


4) Ashley Cole Baada ya kuondoka kwa utata mkubwa kwenye klabu ya Arsenal in 2006, Cole alitukanwa mno na mashabiki wa Arsenal - njia pekee ya kuwajibu aliyoiona Cole ilikuwa ni kucheza mpira mkubwa na kushinda makombe. 
Alishatwaa makombe kadhaa akiwa na Arsenal, lakini akiwa na Chelsea, beki huyo wa kushoto wa England aliongeza makombe ligi, Champions League na Europa League. 
Pia alishinda ngao ya hisani pamoja FA Cup mara nne na akaongezea taji lingine la Premier league kwenye CV yake.

Ashley Cole lifted the Champions League trophy in 2012
 
 5) Juan Mata Wakati akiwa mmoja wa wachezaji wapya kuwasili darajani, mhispani huyu ndio anayetoa sura ya mbele ya klabu ya Chelsea.
Juan Mata aliwasili akitokea Valencia kwa ada ya uhamisho wa £23.5m  August 2011 na alipewa tuzo ya mchezaji wa mwaka wa klabu baada ya kuisadia timu ya Roberto Di Matteo iliyoshinda ubingwa wa FA Cup na Kombe la mabingwa wa ulaya.
Kijana huyu anatajwa kuwa Gianfranco Zola, msimu uliopita aliiongoza Chelsea kushinda ubingwa wao wa kwanza Europa League. Japokuwa anatajwa kuwa anaweza kuuzwa za Mourinho darajani.

Juan Mata
Share on Google Plus

0 comments: