Mtu mmoja afariki baada ya kutumia dawa za majaribio

Mtu  mmoja  amefariki  na  wengine watano  wako  hospitali baada  ya majaribio  ya  dawa  nchini  Ufaransa kwenda kombo.
Waziri  wa  afya  wa  Ufaransa  Marisol Touraine  amesema leo  kuwa  watu  sita  waliojitolea  kufanya  majaribio  hayo walishiriki  kula  dawa  inayotengenezwa  na  maabara  ya ulaya  kaskazini  magharibi  mwa  mji  wa  Rennes.
Kwa  mujibu  wa  vyanzo karibu  na  mkasa huo, dawa  hiyo ni  ya  kutuliza  maumivu yenye Cannabinoids, kiambato kinachopatikana  katika  mmea  wa  bangi.
Chanzo  kingine  kimesema  kampuni  hiyo  inayofanya utafiti  ilikuwa  inafanya  kazi  hiyo  kwa  niaba  ya  kampuni ya  madawa  ya  Ureno ya Bial.
Waziri  wa  afya  wa  Ufaransa  amesema ajali  mbaya imetokea, na  kuongeza  kwamba  majaribio  hayo yamesitishwa na  watu  wote  waliojitokeza  kuyafanya wametakiwa  kurejea  nyumbani.

Share on Google Plus

0 comments: