Zari hazuiliwa kujifungulia nchini Africa Kusini

 http://api.ning.com/files/DGjgPH8*8vlEceF4cvtpje2xTVgQd*c1zr*mP4g1oNreLMST9DIwM0G6KDVCo31bNArMRy1SXXcIQCoLIJZOGWoEltEQ4NPt/zari2.jpeg


Stop! Mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ amemzuia mama kijacho wake, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ kwenda kujifungulia nje ya Bongo pindi mambo yatakapokuwa tayari.
 “Yaani Diamond hataki kabisa Zari kwenda kujifungulia South Africa (Sauzi). Anataka kila kitu kifanyike hapahapa Bongo. Tayari amemuanzishia kliniki kwenye Hospitali ya AMI (ipo Masaki, Dar),” kilitonya chanzo hicho.
Akizungumzia ishu hiyo, Diamond alisema kuwa anatamani kuwa karibu na mama kijacho wake huyo hivyo ni kweli anataka mwanadada huyo ajifungulie Bongo.

Diamond au Baba Kijacho alisema lengo la kufanya hivyo ni ili iwe shangwe kwa familia nzima tofauti na atakapojifungulia nje ambapo familia italazimika kusafiri kwenda kumuona Chibu Junior.
Kwa mujibu wa Diamond, Zari ambaye ni mama wa watoto watatu akifukuzia huyo wa nne anatarajia kujifungua kati ya mwezi Julai au Agosti, mwaka huu. 
Share on Google Plus

0 comments: