Chelsea mwendo mdundo mbio za ubingwa, yaua ‘kimoko’ ugenini

277DC5B300000578-3035739-image-a-44_1428848506260
Bao la dakika za usiku la Cesc Fabregas limeiwezesha Chelsea kuvuna pointi tatu katika mechi ya ligi kuu soka nchini England ugenini dhidi ya Queens Park Rangers (QPR).
Fabregas alifunga goli hilo pekee dakika ya 88′ katika mechi iliyopigwa jioni ya leo uwanja wa Loftus Road.
Ushindi huo umewafanya Chelsea wazidi kuota mbaya kileleni wakijikusanyia pointi 73, pointi 7 dhidi ya Arsenal wenye pointi 66 katika nafasi ya pili.
Hata hivyo Chelsea wana mchezo mmoja mkononi kwani mechi ya leo ni ya 31 wakati Arsenal wameshacheza mechi 32.
Cesc Fabregas arrives late on to convert Eden Hazard's pass and secure all three points for Chelsea at Loftus Road
BAADA YA CHELSEA KUSHINDA MSIMAMO UKO HIVI
 
Share on Google Plus

0 comments: