Kitengo cha kimataifa cha upelelezi Nchini Urusi FSB, kinasema kuwa
kimewazuilia raia 25 wa Ukraine, kikiwalaumu kwa kupanga mashambulio ya
kigaidi mwezi uliopita wakati jimbo la
Crimea lililoko Ukraine lilipokuwa likiandaa kura ya maoni.
Idara hiyo inasema watu hao
wanaozuiliwa walikuwa wanachama wa vuguvugu la ultra-nationalist na
walikuwa wakijiandaa kusababisha mashambulio hayo katikati na Kusini mwa
Urusi.
Awali, waziri wa usalama wa taifa wa Ukraine, Arsen Avakov amesema
kuwa tume rasmi ya uchunguzi inaonyesha kuwa kitengo maalum cha polisi
kiitwacho Berkut kilichobuniwa kukabiliana na vurumai kiliwauwa
waandamanaji kadhaa katika uwanja wa maandamano mjini Kiev, mwezi
Februari.
Amesema kikosi hicho maalum cha polisi kimevunjiliwa mbali.
Kaimu Waziri mkuu Arseniy Yatsenyuk ameiambia
BBC kuwa rais aliyeng'olewa madarakani Viktor Yanukovych na washirika
wake ndio wahusika wakuu katika maafa hayo.
Zaidi ya watu 100 waliuwawa katika vurumai hilo.
Naye kiongozi mkuu wa upelelezi Nchini Ukrainne
Valentyn Nalyvaychenko amesema kuwa idara ya upelelezi ya Urusi imetuma
tani kadhaa za villipuzi na silaha hadi Ukraine.
0 comments: