Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje ,wa Uganda Henry Okello Oryem, amesema huenda baadhi ya viongozi wa waasi wa M23, wakafikishwa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu kwa tuhuma za kuhusika na uhalifu dhidi ya binaadamu.
Grace Kabogo amezungumza na mchambuzi wa masuala ya kisiasa nchini Uganda, Ali Mutasa,
ambapo kwanza alitaka kujua iwapo hatua hiyo inatokana na shinikizo
lolote kutoka nje, hasa ikizingatiwa kuwa waasi wa M23 walikimbilia
Uganda kwa usalama wao, nchi ambayo imekuwa ikidaiwa kuwasaidia waasi
hao.
Kusikiliza mazungumzo hayo bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini.
Mwandishi: Grace Patricia Kabogo
Mhariri: Mohammed Abdul-Rahman
Kusikiliza mazungumzo hayo bonyeza alama ya spika za masikioni hapo chini.
Mwandishi: Grace Patricia Kabogo
Mhariri: Mohammed Abdul-Rahman
0 comments: