TETEMEKO LA PILI LATOKEA NCHINI CHILE

 


Tetemeko la pili kubwa la ardhi limetokea Kaskazini mwa Chile saa 24 baada ya tetemeko la kwanza kubwa kutokea Jumatano na kuwaua watu sita huku likiharibu nyumba 2,600 huku likisababisha watu kuhamishwa kutoka maeneo ya Pwani.
Tetemeko hilo lenye vipimo vya 7.8 lilimlazimisha Rais Michelle Bachelet kuondoka pwani ya eneo hilo na kuelekea sehemu salama maeneo ya juu.

Maafisa wa huduma za dharura wameamuru kuondoshwa kwa watu kutoka maeneo yaliyo karibu na pwani ya nchi hiyo.
Hii ni baada ya Rais Bachelet alipokuwa kukagua uharibifu uliosababishwa na tetemeko la kwanza Jumatano.
Mawimbi ya kwanza ya Tsunami yamepiga katika fukwe ya bahari na hapajakuwa na taarifa za uharibifu wa aina yoyote.
Serikali za Chile na Peru zililazimika kutoa tahadhari ya tisho la Tsunami kwa mara nyingine ingawa tahadhari hiyo iliondolewa baada ya mawimbi makali kupiga maeneo ya Pwani.
Tetemeko hilo ni kubwa zaidi kuwahi kushuhudiwa ingawa hakuna taarifa zozote za uharibifu zaidi zimeripotiwa.
Share on Google Plus

0 comments: