MAFUNDISHO YA MUNGU NA MTUMISHI WA MUNGU JOSEPHAT .E. MWINGIRA

Photo: Naibariki Jumanne yangu...


DARASA/CHUMBA CHA MAFUNDISHO: ''Mkalimani Mtumishi wa MUNGU Mtume na Nabii Josephat Elias Mwingira, EFATHA MINISTRY.
(Darasa linaendelea lilipoishia...)

"KUTAMBUA ADUI ANAYEKUTAFUNA.

Adui mkubwa wa mtu ni yeye mwenyewe.

Mathayo 7:3 “Basi mbona wakitazama kibanzi kilichoko ndani ya jicho la nduguyo, na boriti iliyoko ndani ya jicho lako mwenyewe huliangalii”.

Yer. 1:11 “Tena Neno la Bwana likanijia kusema Yeremia waona nini, nikasema naona ufito wa mlozi (maana yake ni mateso)”. Sasa mtesi mkubwa ni wewe mwenyewe! YESU anasema liangalie hilo boriti jichoni mwako; yakupasa kufahamu kwamba unatakiwa kuyatatua yale yanayokuhusu kabla hujaanza kuyatatua ya mwingine. Tusiwe watu wa kuangalia huku na huku na kusema, “Yule ana dhambi sana, yule ana shida sana”, hebu uwe mtu wa kuangalia ya kwako halafu uone unaweza kutoka mahali kwenda mahali."

(Usikose Darasa Mwana wa MUNGU huu ni Wakati wako, ni Wakati wako wa kupata Furaha na Amani na Ushindi, ni WAKATI WAKO SASA, Usikose, Ni Neema hii imekujilia, Mshukuru BWANA.)
Share on Google Plus

0 comments: