ARSENAL YAPUGUZWA KASI,STURRIDGE AIONGOZA LIVERPOOL KUIFUNGA EVERTON MABAO 4-0 HUKU JUAN MATA AKIIONGOZA MAN UTD KUPATA USHINDI.


Mshambuliaji wa Liverpool Daniel Sturridge alifunga mabao mawili huku akikosa mkwaju wa penati lakini nahodha Steven Gerrard alikuwa nyota wa mchezo kwenye mechi ya 222 baina ya mahasimu hawa wa kitongoji cha Merseyside,kwenye mchezo Gerrard na Luis Suarez walifunga bao moja moja na kuiongoza Liverpool kuifunga Everton mabao 4-0.
 


Arsenal ilishindwa kujikita kileleni baada ya kulazimishwa sare ya mabao 2-2 na Southampton ugenini kwenye uwanja wa St Mary’s.



Mchezaji ghali kwenye historia ya klabu ya Man Utd Juan Mata alivaa jezi yake namba 8 ya Man Utd kwa kuiongoza timu hiyo kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Cardiff City.
Kwenye mchezo huo mabao ya Man U yalifungwa na Robin Van Persie pamoja na Ashley Young.
Share on Google Plus

0 comments: