TULITENGWA MAONI YA SHERIA YA MABADILIKO KATIBA MPYA


Unaweza kujiuliza nani anasema kweli katika hili, hakuna shaka jibu litapatikana
Dar es Salaam. Wiki mbili baada ya Rais Jakaya Kikwete kukutana na viongozi wa vyama vya CCM, Chadema, CUF, NCCR Mageuzi na UDP Ikulu mjini Dar es Salaam na kukubaliana mambo mawili makubwa kuhusu Muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, vyama visivyo wa uwakilishi bungeni vimeeleza kuwa havikushirikishwa katika kikao hicho.
Viongozi wa vyama hivyo vidogo waliibua hoja hiyo katika mkutano kati ya viongozi wa vyama vya siasa na Msajili wa Vyama vya Siasa, Jaji Francis Mutungi uliofanyika Dar es Salaam, kueleza kuwa Rais Kikwete alitoa kauli ya kutaka vyama vyote viwasilishe maoni, hakubagua chama chochote cha siasa.
Katika mkutano huo wa ndani, viongozi hao walimrushia  makombora mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba wakidai kuwa yeye na wenyeviti wenzake wametoa maoni ya vyama vyao, siyo ya vyama vyote 20 vya siasa vilivyopo nchini na kwamba hawakushirikishwa.
Mwenyekiti wa Baraza la Vyama vya Siasa, Peter Kuga Mziray (PPT Maendeleo) anasema kutokana na hali hiyo vyama  hivyo navyo vimeomba kuonana na Rais Kikwete ili kutoa maoni yake.
Jaji Mutungi kwa upande akalazimika  kutumia busara kupoza mvutano huo, huku akivionya vyama hivyo kujenga utaratibu wa kushirikishana katika kila jambo.
Katika mkutano wa Bunge uliopita wabunge wa Chadema, CUF na NCCR-Mageuzi walisusia mjadala wa muswada huo bungeni  wakipinga matayarisho yake kutoshirikisha upande wa Zanzibar na pia walikuwa hawakubaliani na baadhi ya vipengele vya muswada huo.
Baada ya muswada huo kupitishwa, vyama hivyo viliungana na kutangaza kufanya maandamano makubwa, Oktoba 10 mwaka huu, ambayo hata hivyo hayakufanyika baada ya Rais Kikwete kuwaita Ikulu wenyeviti wa vyama hivyo na hatimaye kukubaliana.
Rais Kikwete na viongozi wa vyama hivyo walikubaliana kwamba vyama vyote vya siasa nchini vyenye mawazo, maoni na mapendekezo ya kuboresha Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba viwasilishe mapendekezo yao haraka serikalini ili ifafutwe namna ya kuyashirikisha mapendekezo hayo katika marekebisho ya sheria hiyo.
Pia, walikubaliana kuwa  vyama vya siasa nchini viangalie namna ya kukutana na kujenga mfumo wa mawasiliano na maridhiano ili kusukuma mbele mchakato huo kwa masilahi mapana ya nchi huku, huku Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD)  kikipewa jukumu la kuandaa mkutano wa vyama hivyo na wadau wengine nchini.
Hali ilivyokuwa
Akitoa ufafanuzi wa jinsi vyama visivyo wa uwakilishi bungeni vilivyotoswa kutoa maoni yao, Mziray anasema: “Vyama vyetu ndani ya TCD vinawakilishwa na mwenyekiti wa UPDP, Fahm Dovutwa.
Share on Google Plus

0 comments: