MAMBO yameendelea kuwa magumu katika
hatua za mwanzoni kwa kocha David Moyes, baada ya leo Manchester United
kuchapwa mabao 3-1 na Sevilla katika mechi maalumu ya kumuaga Rio
Ferdinand Uwanja wa Trafford.
Katika mchezo huo ulioshuhudiwa na
mashabiki zaidi ya 40,000, mabao ya Sevilla yamefungwa na Perotti dakika
ya 21, Marin dakika ya 25 na Rabello dakika ya 91, wakati bao la kufutia machozi la United limefungwa na Valencia dakika ya 65.
Kikosi cha Manchester United kilikuwa; De
Gea, Fabio, Ferdinand, Smalling, Buttner, Valencia/Carrick dk65,
Anderson/Giggs dk65, Cleverley/Jones dk46, Januzaj, Kagawa/Zaha dk65 na
Henriquez/Lingard dk46.
Sevilla: Beto, Figueiras, Fazio, Pareja/Puerto dk56, Alberto, Medel, Kondognbia, Marin, Perotti, Vitolo na Bacca.
Kuaga: Rio akiwapungia mkono mashabiki wa United kabla ya kuanza kwa mechi na Sevilla
Kocha mpya wa United, Moyes akisaini autographs wakati anaingia uwanjani
Asante kwa kuja: Rio akiwapungia mikono mashabiki wakati anaingia uwanjani Old Trafford
Marin akifunga
Vitolo akifunga bao la kwanza dakika ya 21
Ferdinand akiwa na Rais wa Sevilla FC, Jose Maria del Nido kabla ya mechi
Mashabiki wakiwa na picha za Rooney, ambaye anataka kuondoka.
0 comments: