Childress
ni msaidizi wa Obama katika Ikulu ya Marekani (White House) akiwa Naibu
Mkuu wa Utumishi anayeshughulikia mipango katika Serikali ya nchi hiyo
na aliwahi kufanya kazi katika Bunge la Seneti.
Obama
amefanya uteuzi huo ikiwa ni wiki moja tangu alipohitimisha
ziara yake
katika nchi tatu za Bara la Afrika, ikiwemo Tanzania.
Taarifa
iliyotolewa na Ikulu ya Marekani ilisema nafasi hiyo inahitaji
kuidhinishwa na Bunge la Seneti la nchi hiyo kwa sababu uteuzi wake
unaweza kuwa na maana kubwa katika kutekeleza sera za nje za Marekani.
Kuteuliwa
kwa Childress kunaashiria kwamba Balozi wa sasa wa Marekani nchini
Alfonso Lenhardt anakaribia kumaliza muda wake, awali Childress ambaye
aliwahi kuwa msaidizi na msiri wa muda mrefu wa Seneta wa zamani Tom
Daschle, alitarajiwa kushika moja ya nyadhifa mbili katika utawala wa
Rais Obama ambazo ni Mkuu wa Utumishi katika Idara ya Huduma ya Afya ya
Jamii (HHS) au Naibu Mkurugenzi katika Ofisi ya Maboresho ya Afya katika
Ikulu ya Marekani.
0 comments: