Jambo ambalo hakulitaja pengine kwa makusudi au kwa bahati mbaya ni ukweli kwamba upungufu wa wanafunzi wa kujiunga na kidato cha tano mwaka huu utakuwa mkubwa zaidi kwa kuwa zaidi ya robo ya wanafunzi waliochaguliwa kuingia katika sekondari na vyuo vya Serikali watajiunga na sekondari za watu binafsi.
Takwimu zilizotolewa juzi na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya
Ufundi kuhusu wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano
katika sekondari za Serikali na vyuo vya ualimu mwaka huu zinasononesha
na zimethibitisha pasipo kuacha shaka kwamba nchi yetu inaelekea kuzimu
katika suala zima la elimu.
Hatuhitaji kupiga ramli kujua kwamba Serikali
isipochukua hatua stahiki haraka iwezekanavyo, hata mafanikio kiduchu
tuliyokwisha kuyapata yatapotea na kuiacha sekta nzima ya elimu ikiwa
mfu. Tunasema hivyo kutokana na takwimu za kutisha zilizotangazwa na
wizara hiyo juzi kuonyesha kwamba kutakuwa na upungufu wa wanafunzi
10,074 wa kidato cha tano katika sekondari zinazomilikiwa na Serikali.
Picha halisi ni mbaya zaidi kuliko ile
iliyoonyeshwa na Naibu Waziri wa wizara hiyo, Philipo Mulugo wakati
alipotangaza uteuzi wa wanafunzi hao katika mkutano wake na waandishi wa
habari juzi. Jambo ambalo hakulitaja pengine kwa makusudi au kwa bahati
mbaya ni ukweli kwamba upungufu wa wanafunzi wa kujiunga na kidato cha
tano mwaka huu utakuwa mkubwa zaidi kwa kuwa zaidi ya robo ya wanafunzi
waliochaguliwa kuingia katika sekondari na vyuo vya Serikali watajiunga
na sekondari za watu binafsi. Hivyo, hapa tunazungumzia upungufu wa
wanafunzi wapatao 13,000 hivi.
Kwa hiyo, tunaishauri Serikali ilione tatizo
hilo katika mapana yake, kwa maana ya kuliona kama janga la kitaifa na
kulifanya kipaumbele cha kwanza katika mipango ya maendeleo. Elimu ni
suala mtambuka kwa sababu inagusa kila sekta, zikiwamo nishati, maji,
miundombinu na kilimo ambazo zimetajwa kuwa vipaumbele vya Serikali
katika mwaka huu wa fedha. Ndiyo maana tunasema fedha zinazotengwa kila
mwaka kwa ajili ya elimu zisipungue asilimia 30 ya bajeti ya Serikali na
hili linawezekana iwapo tu tutapunguza vipaumbele ili mkazo uwekwe
kwenye elimu.
Lazima tufike mahali tukiri kwamba moja ya
changamoto kubwa zinazotukabili kama taifa ni kushuka kwa viwango vya
elimu kwa kasi ya kutisha. Takwimu zilizotolewa na
Serikali juzi kuhusu ufaulu wa wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya ualimu hazitoi taswira nzuri ya mfumo wetu wa elimu, kwani vigezo vya kujiunga na taasisi hizo viko chini mno, ingawa nafasi nyingi hazikujazwa kutokana na wanafunzi wengi kushindwa hata kufikia vigezo hivyo vya chini.
Serikali juzi kuhusu ufaulu wa wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano na vyuo vya ualimu hazitoi taswira nzuri ya mfumo wetu wa elimu, kwani vigezo vya kujiunga na taasisi hizo viko chini mno, ingawa nafasi nyingi hazikujazwa kutokana na wanafunzi wengi kushindwa hata kufikia vigezo hivyo vya chini.
Ni maeneo gani tumeendelea kufanya makosa?
Tumeendelea kupeleka katika vyuo vya ualimu wanafunzi ambao hawakufanya
vizuri katika mitihani ya kidato cha nne. Nchi zinazothamini elimu
hupeleka katika vyuo vya elimu wanafunzi waliofanya vyema katika
mitihani ya sekondari, hasa ya kidato cha sita. Sisi tumeendelea kufanya
makosa kwa kupeleka wanafunzi walioshindwa kidato cha nne kusomea
ualimu, kwani hawawezi kujenga misingi mizuri kwa watoto na badala yake
wanaporomosha viwango vya elimu.
Kwa jumla, kutokuwapo wanafunzi wa kutosha
kujaza nafasi za kidato cha tano katika sekondari 207 za Serikali pamoja
na kupeleka walioshindwa kidato cha nne kusomea ualimu ni hali
itakayosababisha janga kubwa kwa nchi yetu katika siku za usoni. Sasa
tutazamie vyuo vikuu kukosa wanafunzi na vile vya binafsi kufungwa, huku
tukibaki nyuma kielimu tofauti na wenzetu. Hayo ndiyo matokeo ya kuipa
elimu kisogo miaka nenda miaka rudi.
CHANZO MWANANCHI
CHANZO MWANANCHI
0 comments: