POLISI WALIONASWA WAKISAFIRISHA MAGUNIA BANGI ARUSHA WATWAJWA

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas (pichani), amewataja polisi wawili na gari la jeshi hilo ambalo walilitumia kusafirisha magunia 18 ya bangi kwenda Holili mpakani mwa Tanzania na Kenya. Aliwaja wkuwa ni dereva wa gari hilo Koplo Edward lenye namba za usajili PT 2025 aina ya Toyota Landcruiser linalotumiwa na Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) mkoani hapa, na mwenzake PC George namba za polisi G 2434.
Watuhumiwa hao wanatarajiwa kufikishwa mahakama ya kijeshi baada ya....... taratibu kukamilika.
Kamanda Sabas alisema jeshi hilo lilipata taarifa kutoka kwa raia wema kuhusu baadhi ya polisi wanaojihusisha na biashara hiyo tena kwa kutumia magari ya serikali.
Alisema baada ya taarifa hizo, walijipanga kwa kushirikiana na wenzao
wa mkoani Kilimanjaro na kuweka mtego uliofanikisha kuwanasa saa 5:00 usiku wakiwa katika Mji mdogo wa Himo.
Alisema gari walilokuwa wakiendesha lilikuwa limesheheni magunia 18 ya bangi ambayo walikuwa wakiyasafirisha kwenda Holili kwa lengo la kuuza kwa wafanyabiashara wa nchi jirani.
BY JOHN NGUNGE
SOURCE: NIPASHE

Share on Google Plus

0 comments: