Dar es Salaam. Sakata la Mkuu wa Itifaki wa Ikulu, Anthony
Itatiro, ambaye anahusishwa na njama za kutaka kuchota kiasi cha Sh3
bilioni kwa ajili ya safari hewa ya Rais, limechukua sura mpya baada ya
Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje kutaka ku......
jua hatima ya kigogo huyo jana.
jua hatima ya kigogo huyo jana.
Itatiro na maofisa wanne wa Wizara ya Mambo ya
Nje na Ushirikiano wa Kimataifa walituhumiwa mwaka jana kuidhinisha
kuchota kiasi hicho cha fedha bila ya kuwapo kwa ziara ya Rais kwenda
nchi yoyote ya kigeni.Mpango huo unadaiwa kusukwa Juni mwaka jana kwa maofisa
haokuitaka Wizara ya Fedha kutoa kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya
safari hewa ya Rais.
Naibu Waziri wa wizara hiyo, Juma Mahadhi
alitoa maelezo hayo baada ya kuulizwa swali na Mwenyekiti wa Kamati ya
Mambo ya Nje ya Bunge, Edward Lowassa.HABARI NA MWANANCHI
0 comments: