MDAHALO WA MWISHO WA WAGOMBEA UCHAGUZI WAMALIZIKA JANA JIONI


Awali kulikuwa na taarifa kuwa mgombea wa Urais Uhuru Kenyatta alikuwa amesusia mdahalo huo akidai kuwa mdahalo wa kwanza waliokuwa wanauendesha mjadala wenyewe waliangazia sana swala la ICC na kuwafanya wagombea wengine kumlemea.
Uhuru pamoja na mgombea mwenza William Ruto, wanakabiliwa na kosa la kuwa washukiwa wakuu wa ghasia za baada ya uchaguzi mkuu mwaka 2007/2008 katika mahakama ya ICC. Duru zilisema kuwa Uhuru alisitisha kampeini zake leo ili kuweza kujiandaa vilivyo kwa mjadala huo.
Wagombea wengine akiwemo waziri mkuu Raila Odinga wanajiandaa kwa mjadala huo ambaop hii leo utalipa kipao mbele mbele swala la ardhi, sera za kigeni, na uchumi.

Share on Google Plus

0 comments: