Awali kulikuwa na taarifa kuwa mgombea wa Urais Uhuru Kenyatta
alikuwa amesusia mdahalo huo akidai kuwa mdahalo wa kwanza waliokuwa
wanauendesha mjadala wenyewe waliangazia sana swala la ICC na kuwafanya
wagombea wengine kumlemea. Uhuru pamoja na mgombea mwenza
William Ruto, wanakabiliwa na kosa la kuwa washukiwa wakuu wa ghasia za
baada ya uchaguzi mkuu mwaka 2007/2008 katika mahakama ya ICC.
Duru zilisema kuwa Uhuru alisitisha kampeini zake leo ili kuweza kujiandaa vilivyo kwa mjadala huo. Wagombea wengine akiwemo waziri mkuu Raila
Odinga wanajiandaa kwa mjadala huo ambaop hii leo utalipa kipao mbele
mbele swala la ardhi, sera za kigeni, na uchumi.
0 comments: