WAIRAN WAWILI WAFUNGWA KIFUNGO CHA MAISHA KENYA

iran_terrorists

Raia wawili wa Iran wamehukumiwa kifungo cha maisha katika mahakama moja ya 
Kenya kuhusiana na mashtaka ya ugaidi.Raia hao ni Ahmad Mohammed na Sayed 
Mousavi ambao walishtakiwa wiki iliyopita kwa kumiliki..... vilipuzi, ambavyo 
 inaaminika vilikuwa vitumiwe kwa kufanya mashambulizi."mwili unanisisimka 
nikifikiria hasara ambayo ingesababishwa na shambulizi hilo la kigaidi," amesema 
jaji Kiarie Waweru Kiarie, kama linavyoripoti shirika la habari la AFP.Hata hivyo, 
serikali ya Iran imekana kuhusika na mpango huyo wa kuishambulia nchi ya Kenya.  
Siku ya Jumapili, balozi wa Iran nchini Kenya, Malik Hussein Givzad, amesema
 ubalozi utasaidia familia za washtakiwa hao ku......kata rufaa dhidi ya hukumu iliyotolewa.
"kama ubalozi, tunachoweza kufanya ni kuzisaidia familia za washtakiwa 
kukata rufaa, iwapo mawakili wanahisi kwamba hakuna ushahidi wa 
kutosha," amenukuliwa balozi Givzad na gazeti la Kenya Daily Nation.
"nchi ya Iran ina uhusiano mzuri wa kibiashara na Kenya. Huu ulikuwa ni 
mchakato wa kisheria, tunauheshimu." ameongeza kusema.
Mahakama ilibaini kwamba Mohammed na Mousavi ambao 
wanahusishwa na mtandao ambao unapanga njama ya kulipua mji wa 
Nairobi na sehemu ya pwani ya nchi hiyo Mombasa.
Jaji Kiarie amesema ameamua kuwafunga maisha kwa sababu ya vilio vya 
waathirika wa milipuko iliyopita vilisikika zaidi kuliko kujitetea kwao, imeripoti AFP.
Mawakili kutoka upande wa utetezi wanadai kwamba, Mohammed na Mousavi 
walihojiwa na maafisa wa usalama wa Israel pindi walipokuwa wanashikiliwa.
Hata hivyo, upande wa mashtaka umekana tuhuma hizo.
Share on Google Plus

0 comments: