MILIONI 50 KUTOLEWA KWA ATAKAEMTAJA MLIPUAJI BOMU ARUSHA

Mkuu wa jeshi la polisi nchini ameahidi kutoa zawadi nono ya fedha taslim za kitanzania sh.milioni50 kwa yeyote atakae toa taarifa za kuwafichua wahalifu wengine wa tukio la mlipuko ulio tokea katika kanisa la Roma  lililopo Olasiti.
hayo yamebainishwa na kamanda wa polisi mkoa wa Arusha ACP Liberatus Sabas aliopokua akiongea na waandishi wa habari juu ya taarifa za kukukamatwa kwa wahalifu walio......
fikia 13 ambapo wahalifu wa nne wakiwa ni raia wa falme za kiarabu.
Kamanda Sabas amesema kuwa watuhumiwa 10 kati yao tayari washaojiwa na wanatarajiwa kufikishwa mahakani mda wowote huku watatu kati yao bsdo wanaojiwa naendapo upelelezi utakamililka watafikishwa pia mahakamani
Hata hivyo taarifa zinasema kuwa kabla ya uzinduzi wa kanisa la Romani Katoriki parokia mpya ya Olasiti ambapo mgeni rasmi alikuwa barozi wa Vatican nchini Askofu Francisco Padilla alipokuwa anataka kukata utepe wa uzinduzi ndipo mtu mmoja aliekuwa amejificha kwenye choo kilicho jirani na kanisa hilo umbali wa mita 20 alirusha bomu hilo
Aidha Kamanda Sabas amefafanua kuwa bomu hilo lilileta madhara kwa watu wapatao 66 ambapo watatu kati yao warifaliki wakiwa kwenye taratibu za matibabu na hivyo wanatarajiwa kuzikwa kesho May 10 katika kanisa hilo la Olasiti Pamoja na hayo kamanda amewahakikishia wakazi wa jiji Arusha kuwa ulinzi umeimarishwa vyakutosha hasa kwenye zile sehemu zenye mikusanyiko mikubwa kama huo unaotarajiwa kesho kwenye mazishi.
 
STORI NA HAZLA QUIRE


Share on Google Plus

0 comments: