ULINZI MKALI WAWEKWA KATIKA SHEREHA YA PAPA

Add caption


Vatican City. Ulinzi mkali umeandaliwa kwa viongozi mbalimbali wa kiserikali na wale wa kidini duniani waliowasili jijini Vatican, kwa misa maalumu ya kutawazwa kwa Papa Francis leo.

Waumini na wageni milioni moja akiwamo Balozi wa Tanzania nchini Italia, Dk James Msekela, wanatarajiwa kuhudhuria misa hiyo itakayofanyika kwenye Viwanja vya Kanisa Kuu la Mtakatifu Petro.

Baada ya Papa Francis kutawazwa, ataanza rasmi kazi ngumu ya kuliongoza Kanisa Katoliki lenye waumini wengi na ambalo limekumbwa na mizozo kadhaa ikiwamo ya utovu wa nidhamu kwa baadhi ya makasisi.

Kiongozi huyo alichaguliwa Jumatano iliyopita kuchukua nafasi iliyoachwa wazi na Papa Benedict XVI, aliyejiuzulu Februari 28, mwaka huu.

Misa ya kutawazwa kwa Papa Francis, imeifanya Mamlaka ya Jiji la Rome kuandaa ulinzi mkali kwa watu wote ambao wanatarajiwa kuhudhuria tukio hilo la kihistoria.
Tayari, Papa Francis ameduwaza wengi kwa kauli na vitendo vyake vingi ambavyo vinamwonyesha kama kiongozi asiyependa makuu na ambaye pia anatarajiwa kubadili uendeshaji wa kanisa hilo lenye waumini 1.2 bilioni.
Share on Google Plus

0 comments: