WE WISH YOU A WONDERFUL, LOVELY $ HAPPY NEW YEAR 2014...STAY CALM

Uongozi wa HABARI KAMILI KAMILI unawatakia wasomaji wote wablog yetu endelea kupata habari motomoto huku ukisherekea mwaka mpya MUNGU awalinde na kuwafikisha salama mwaka 2014 AMEEEEEEEN.....

0 comments:

KILI STARS YAIVUA UBINGWA UGANDA NA KUTINGA NUSU FAINALI - KUKIPIGA NA HARAMBEE DEC 10

Timu ya Kilimanjaro Stars leo hii imefanikiwa kufuta uteja kwa Uganda baada ya kuifunga timu hiyo katika mchezo wa robo fainali ya kombe la CECAFA Challenge Cup.

Mchezo huo wa robo wa fainali uliochezwa jioni ya leo Kili Stars imefanikiwa kuivua ubingwa The Cranes na kuingia robo nusu fainali baada ya kushinda mikwaju ya penati 3-2 huku kipa Ivo Mapunda akiibuka kuwa shujaa.


Katika dakika 90 timu hizo zilitoka sare ya bao 2-2, Stars walianza kuongoza kwa mabao mawili yaliyofungwa na Mrisho Ngassa, lakini Uganda wakasawazisha kupitia Sserunkuma Dakika ya 16 na Martin Mpuga kipind cha pili katika dakika 73.
Kwa matokeo hayo Kilimanjaro Stars itamenyana na wenyeji, Kenya, Harambee Stars katika Nusu Fainali ya Kwanza ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge Desemba 10, mwaka huu Uwanja wa Nyayo, Nairobi, Kenya.

0 comments:

MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA AWATAKA WANA ARUSHA KUACHA USHABIKI WA KISIASA UNAOHATARISHA AMANI

 
Msajili  wa vyama vya siasa  nchini  Bw Fransis  Mutungi  amewataka  wananchi  wa  Mkoa  wa  Arusha na watanzania  kwa  ujumla   kuepuka kuingiza  ushabiki  kwenye  siasa  kwani   kufanya  hivyo  licha ya kuwa  chanzo   cha kuhatarisha  amani  wanaharibu   lengo  la  fani hiyo  ambayo ina  umuhimu  na  faida  kubwa  katika  jamii   kama  taratibu  na misingi yake  ikifuatwa   na kuheshimiwa .
Akizungumza  na wananchi na viongozi wa  ngazi mbalimbali  za  Mkoa  wa  Arusha  waliokusanyika  katika  uwanja  wa  Shekh Amri  Abeid  kuuombea mkoa  wa Arusha amani  Bw  Mutungi  amesema amani ndio msingi  wa  kila  kitu  na  haihusiani kabisa  na  siasa hivyo  hakuna sababu ya  watanzania  kukubali  amani  iliyopo ivurugwe  na  watu  wachache  wanaosingizia  siasa  kwani  wanaopenda amani  ni  wengi  kuliko  wanasiasa 
 
Wakizungumza  katika  hafla hiyo   viongozi wa ngazi mbalimbali  akiwemo   shekh mkuu  wa  mkoa   shabani  bin jumaa  na  askofu  mkuu  wa  kanisa  la  evengelisim centre   eliud  wamewaomba  viongozi  wa  kisiasa  na  wanaotarajia  kutafuta  nafasi za  uongozi   kuwajengea  wananchi  utamaduni  wa  kuheshimi  sheria    na  dola  iliyoko madarakani  kwani    wakizoea  kuvunja  sheria   watafanya hivyo  hata  uongozi  ulioko  madarakani ukibadilika .
 
Mkuu wa  mkoa  wa   arusha  Bw  Magesa  Mulongo  amesema  upo uwezekano  wa  kuendesha  siasa, kudai  haki    na  hata  kukosoa na kutoa  mapendekezo   bila  kuvuruga amani.
 
Wananchi hao  wakiwa  na viongozi wa  ngazi mbalimbali  wakiwemo  wa  kisiasa ,viongozi wa dini  na  wa  mila  walikusanyika katika uwanja   huo  kuhubiri na  kuuombea  mkoa  wa  arusha  amani  unaoandamwa  na  heka heka za  kisiasa  ambazo zimesababisha  kuyumba kwa  uchumi.

-ITV

0 comments:

DK SLAA NA MBOWE APOKELEWA KWA MABANGO YA KUJIUZULU MKOANI KIGOMA


Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Wilbrod Slaa amepokewa kwa mabango katika mkutano wake wa hadhara wilayani Kakonko, Kigoma lakini akawaambia waliofanya hivyo kuwa chama chake hakitayumbishwa huku akiwataka wanaosimama na mabango kumtetea Zitto Kabwe kung’oka naye ndani ya chama.

Dk Slaa yuko mkoani Kigoma ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku 11 kutembelea Mikoa ya Shinyanga na Kigoma kukagua na kuimarisha uhai wa chama.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa Mwenge Kakonko, Dk Slaa alisema Chadema ni chama imara na kinaendeshwa kwa misingi ya katiba na kanuni.
“Hakuna kiongozi aliye juu ya katiba, ninawaasa wote wanaobeba mabango kujiangalia kwa kuwa ninafahamu wanatumiwa.”

Kabla ya kupokewa kwa mabango hayo, Dk Slaa aliyewasili Kakonko saa 5:11 asubuhi akitokea Wilaya ya Kahama, Shinyanga alikwenda moja kwa moja katika Kata ya Mhange ambako alifanya mkutano wa hadhara.
Dk Slaa alikumbana na mabango hayo saa 8:45 mchana msafara wake ulipowasili Kakonko Mjini ukitokea Mhange.
Wakati Dk Slaa akiingia katika uwanja wa mkutano, ulio jirani na Ofisi za CCM Wilaya ya Kakonko, kuliibuka kundi la vijana wapatao watano wakiwa na mabango mkononi na kuanza kukimbia kuyafuata magari matatu ya msafara wa Dk Slaa huku wakionyesha mabango yao. Hatua hiyo iliwafanya polisi waliokuwapo eneo hilo la mkutano kuwazuia na kuanza kuwatimua lakini mara baada ya Dk Slaa kuteremka katika gari yake na kuingia uwanjani hapo, aliomba kipaza sauti na kuwataka askari hao kuacha kuwatimua wenye mabango. “Naomba msiwaondoe waacheni waje... waruhusuni kwenye mkutano na mabango yao. Waacheni waje hapa … msiwazuie, waacheni waonyeshe mabango yao na muwaruhusu tu wapite hapa mbele, msiwapige tafadhali,” alisema Dk Slaa.
Baada ya kauli hiyo, polisi waliwaruhusu vijana hao watano ambao walibakiwa na mabango manne, moja likiwa limechanika walipokuwa wanawazuia.
Mabango hayo yaliyokuwa na maandishi ya aina moja, yalikuwa na ujumbe uliosomeka: “Tanzania Kigoma Kakonko bila Zitto Haiwezekani”, ‘Mhe. Slaa, Mhe. Mbowe mnatakiwa kujiuzuru mara moja” na jingine lilisomeka; “Hatupo tayari kwa kusikiliza lolote bila ya Zitto”.
Mara baada ya kupanda jukwaani Dk Slaa aliwataka tena wenye mabango kusogea karibu na jukwaa kuu alipokuwa amesimama na kuanza kuwauliza maswali vijana hao iwapo wanajua Katiba ya Chadema na kama wana kadi za chama. “Naomba niwaulize, hivi nyie wenye mabango mnaijua Katiba ya Chadema?” Walimjibu: “Hapana.” Dk Slaa akawauliza tena: “Sasa mnadai nini kwa mabango yenu kama hamjui Katiba ya Chadema?”
Mmoja wa walioshika mabango hayo alijibu: “Mtetezi wetu Zitto.”
Kutokana na hali hiyo Dk Slaa aliwauliza, atakuwa amekosea akiwakabidhi kwa Polisi kuwa siyo wanachama wa Chadema lakini wanafanya vurugu katika mkutano halali?

0 comments: