NAPE NNAUYE AYAKANA MATUSI YAKE KWA WAZEE


Nape Nnauye ameamua kuvunja ukimya na kutoa utetezi wake kuhusu kauli yake chafu iliyochapishwa na gazeti la Mtanzania likimtuhumu kuwatusi wazee waliopendekeza uwepo wa serikali tatu.....

Huu ni utetezi wake:

"Nimestushwa sana na stori ya gazeti la Mtanzania inayodai kuninukuu kuwa nimesema wazee waliopendekeza serikali tatu wanasubiri kufa!

Kwakweli nimesikitishwa sana hata na jinsi maneno ndani yalivyopangiliwa kiasi kwamba inanipa tabu kuamini kama mhariri aliipitia hii stori ukiachilia mbali kama aliyetumwa kuja kuandika stori alikuwa ni "too junior"

0 comments:

JACK WOLPER AMJIBU MBAYA WAKE ALIYETANGAZA KUWA YEYE NI KAHABA


Msanii nyota wa filamu bongo, Jacqueline Wolper amewataka wasanii wa bongo movie kuacha tabia ya kupigana majungu ya kinafiki ambayo huchangia kujenga bifu za kijinga....

Akiongea na mpekuzi wetu, wolper alidai kuwa kuna mipaka ya watu kuishi lakini kuna baadhi ya wasanii wanaamini kwamba majungu ndo mshahara wao kiasi kwamba wasipomsengenya mtu basi hawawezi kuishi...

Wolper anadai kuwa yeye ni miongoni mwa wasanii wanaosemwa sana kwa mabaya hasa kuhusu maisha yake ya kila siku.Hali hiyo inatokana na umaarufu alionao ambao huwafanya wasanii wenzake wamchukie hasa wasanii wa kike...



Hii ni kauli ya Wolper alipoongea na mpekuzi:

"Wasanii tungekuwa na ushirikiano kama nisha tungefika mbali sana.

"Mimi simuogopi mtu katika maisha yangu, lakini

0 comments:

MSHIRIKI WA TANZANIA ( NANDO ) ATIMULIWA BIG BROTHER BAADA YA KUGOMBANA NA MSHIRIKI MWENZAKE


Jana usiku mara tu baada ya Sulu na Annabel kutolewa kwa kura za watazamaji, Big Brother aliwaita washiriki pamoja katika kikao cha dharura kufuatia ugomvi uliotokea kati ya Nando na Elikem.

Itakumbukwa kwamba siku ya ijumaa ilitokea hali ya kutoelewana kati ya Nando na Elikem. Wawili hawa walitukanana sana na kutishiana mno. Ugomvi huo ulianzishwa na Nando.

Kwa mujibu wa sheria za Big Brother mwaka huu, kuanzisha ugomvi ni kosa ambalo hupelekea kupata 'strike' ama onyo.

3 strike rule ni mtindo unaotumika msimu huu. Kwa mujibu wa Big brother, yeyote atakaye fanya makosa matatu makubwa

0 comments:

AGNESS MASOGANGE AFUTIWA DHAMANA YAKE NA KURUDISHWA RUMANDE


HUKU akiwa hajui nini hatima ya kesi inayomkabili ya kunaswa na madawa ya kulevya nchini Afrika Kusini, Video Queen Agnes Gerald ‘Masogange’ amepata balaa jipya

Kwa mujibu wa chanzo chetu makini ambacho kipo nchini humo, Masogange na mwenzake aliyekamatwa naye, Melisa Edward wamefutiwa dhamana hivyo wamerudi tena rumande.

Habari zinadai kuwa, dhamana za wawili hao zimefutwa kufuatia kuhisiwa kwamba wana mpango wa kuondoka nchini huko kinyemela na kurejea Tanzania, jambo ambalo limetafsiriwa kama jaribio la kuikimbia kesi hiyo.


“Unajua huku Sauzi si kila mtu anawaonea huruma Masogange

0 comments:

"NIPO TAYARI KUJIUZULU ENDAPO ITABAINIKA NAUZA MADAWA YA KULEVYA'.....MBUNGE WA CCM (AZZAN) AFUNGUKA


MBUNGE wa Kinondoni (CCM), Idd Azzan, amesema yupo tayari kujiuzulu ubunge, ikiwa itabainika anajihusisha biashara ya dawa za kulevya. Kauli hiyo imekuja siku chache baada ya kutajwa katika moja ya barua iliyosambazwa katika mitandao ya kijamii, baada ya mtu anayedaiwa kukamatwa China na kuwatuhumu watu kadhaa akiwamo Idd Azzan.

Akizungumza na MTANZANIA jana kuhusu sakata hilo, alisema hatua ya kuhusishwa na biashara haramu ya dawa za kulevya, ni kutotenda haki mbele ya jamii hasa wapiga kura wake na Taifa kwa ujumla.

Alisema mtu aliyendika barua ya tuhuma dhidi yake, ni wazi amedhamiria kumshushia heshima na huenda akawa ana jambo limejificha.

“Ni kweli nimeiona hiyo barua katika mtandao, inayodaiwa imeandikwa na kijana ambaye amekamatwa Hong Kong nchini China. Lakini ninajiuliza kama kweli yeye ni raia mwema, katika hili kwanini hakutaka kutaja jina lake kwenye barua hiyo.

“Hata nilipoisoma nimebaini kuwa huyo mtu ametumika na huenda kabisa hayupo nje ya nchi, kwani katika maelezo yake anataja jina la Balozi Philip Marmo kuwa amemsaidia hali ya kuwa hivi karibuni Rais Kikwete alimteua Balozi mpya Abdulrahman Shimbo na Marmo kuwa Balozi wa Shirikisho la Ujerumani.

“Kingine naona alijaribu kuandika uongo kuweza kuaminisha jamii, kwani hata hilo jila la balozi mwanzo limetajwa jina la Bernad na kukatwa kwa wino. Ninapenda kulieleza Taifa kuwa naomba vyombo vya usalama vifanye uchunguzi wa jambo hili na nikibainika ninauza dawa za kulevya nipo tayari kujiuzulu ubunge wangu.

“Kubwa haki itendeke katika kufanya uchunguzi wa jamb

0 comments:

MAREKANI YAMPA ONYO RAIS KAGAME WA RWANDA....YAMTAKA KUACHA MARA MOJA KUWASAIDIA WAASI WA M23


Marekani imeitaka Rwanda kuacha kusaidia waasi wa kundi la M23 ambalo linaendesha mapambano dhidi ya Serikali ya nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).

Taifa hilo kubwa duniani limesema lina ushahidi wa kutosha kuonesha kuwa Rwanda inalisaidia kijeshi kundi hilo la waasi na baadhi ya maofisa wake wamo.

Hii ni mara ya kwanza kwa Marekani kutoa kauli kali tangu kundi hilo lianzishe mapigano dhidi ya Serikali ya DRC katika mji wa Goma ulioko eneo la Mashariki, ambalo lina utajiri mkubwa wa madini.

"Tunaitaka Rwanda iache mara moja kutoa msaada wa aina yoyote kwa M23," alisema Jen Psaki, Msemaji wa Ikulu ya Marekani. Msemaji huyo pia aliitaka Rwanda iondoe wataalamu wake wa kijeshi ndani

0 comments:

"ATAKAYETHUBUTU KUIVAMIA TANZANIA ATAKIONA CHA MTEMA KUNI. TUPO TAYARI KWA UCHOKOZI WOWOTE"....RAIS KIKWETE ATOA ONYO KALI

Rais Jakaya Kikwete ametuma ujumbe kwa wale wanaoitishia Tanzania. Amewaambia wakithubutu watakiona cha mtemakuni kama ilivyokuwa kwa Idd Amin wa Uganda.
Alisema mamlaka za ulinzi na usalama zilimdhibiti Amin alipofanya uvamizi katika ardhi ya Tanzania mwaka 1978 na kwamba hazitashindwa kufanya hivyo kwa mtu mwingine yeyote atakayechezea usalama wa nchi.
Wakati Rais akisema hayo, Mkuu wa Majeshi, Jenerali Davis Mwamunyange amewahakikishia wananchi kuwa wakati wote jeshi liko imara na kuwataka wasiogope lolote.
Viongozi hao walisema hayo jana katika maadhimisho ya Siku ya Mashujaa iliyofanyika katika Kambi ya Jeshi ya Kaboya iliyopo Muleba, Kagera.
“Sihitaji kusema tena, mmeshamsikia Mkuu wa Majeshi, atakayejaribu atakiona cha mtemakuni, laleni usingizi na msiwe na wasiwasi, msisikilize maneno ya mitaani,” alisema Rais Kikwete na kuongeza:
“Wakati wowote, saa yoyote tuko tayari kulinda nchi yetu. Hatuko tayari kuona amani inaharibika nchini, hatuwezi kuruhusu mtu yeyote kuimega au kuichezea nchi yetu kama alivyofanya Idd Amin.”
Katika siku za karibuni kumekuwa na kauli kadhaa kutoka kwa baadhi ya viongozi wa nchi jirani ambazo zinatafsiriwa na wananchi kwamba ni za kuitisha Tanzania.
Jenerali Mwamunyange alisema jeshi wakati wote liko imara kuwalinda wananchi na nchi kwa jumla hivyo wasiogope...“Endeleeni na shughuli zenu na msiogope mtu yeyote, fanyeni kazi zenu bila wasiwasi.”

Huku akishangiliwa na mamia ya watu waliohudhuria maadhimisho hayo, Jenerali Mwamnyanye alisema yeyote atakayethubutu kuchezea usalama wa nchi atakiona cha mtema kuni.

Akizungumzia Siku ya Mashujaa, Rais Kikwete alisema ni siku ya kuwakumbuka mashujaa waliojitolea maisha yao wakati wa Vita ya Kagera kuilinda nchi yao ili iwe salama na yenye amani.
“Kuhakikisha usalama wa nchi kuna gharama yake kwani kuna wengine walikufa na wengine wakabaki na vilema kwa ajili ya hilo. Wale ambao wamebaki na wana matatizo lazima tuwaangalie vizuri na vile ambavyo havijafanyika tutavishughulikia kwani kutetea taifa ni kazi ngumu.”
Maadhimisho hayo yalihudhuriwa na viongozi mbalimbali wakiwamo, Makamu wa Rais, Dk Gharib Bilal, Rais wa Zanzibar, Dk Mohammed Shein, Jaji Mkuu wa Tanzania, Othman Chande na Jaji Mkuu wa Zanzibar, Omar Othman Makungu ambao wote walipewa nafasi ya kuwasalimia wananchi waliohudhuria maadhimisho hayo.Awali, viongozi wa dini, Askofu Msaidizi wa Kanisa Katoliki Jimbo la Bukoba Methodius Kilaini, Shehe wa Mkoa, Haruna Kichwabuta na Mwakilishi wa Jumuiya ya Makanisa ya Kikristo, Askofu Elisa Buberwa walitoa wito kwa Watanzania kuthamini amani iliyopo na umuhimu wa kuwa na mshikamano katika kuilinda na kuhakikisha kwamba haivurugwi kwa misingi ya imani, itikadi au ukabila.
Matatizo Muleba
Awali, Rais Kikwete aliwahakikishia wananchi wa Muleba kuwa matatizo ambayo wabunge wao wameyawasilisha kwake mbele yao atayashughulikia.
 “Nimesikia yale waliyoyasema hapa ; suala la mpaka kati ya eneo la wananchi na jeshi, Waziri wa Ardhi yupo hapa, kaeni na jeshi na vijiji ili tatizo liishe ni jambo ambalo linawezekana hivyo litatuliwe,” alisema Rais Kikwete.
Alisema suala la umeme na madaraja litashughulikiwa na viongozi wa mkoa wakishirikiana na wabunge na watakapokwama wafikishe kwake... “Mimi ndiye ninayetoa fedha za maendeleo hivyo hayo masuala yakikwama waniambie nitayashughulikia.”

0 comments:

MATUKIO MUHIMU KATIKA MIAKA YA UMOJA WA AFRIKA

AU-Soldaten in Darfur . (AP Photo/Jose Cendon)

Matukio muhimu katika miaka 50 ya Umoja wa Afrika

Ushiriki mpya katika kuleta amani

Mwanzoni mwa karne mpya, asilimia 20 ya wakaazi wa Afrika walikuwa wameathiriwa na vurugu zinazotokana na migogoro. Hivyo amani ilikuwa suala muhimu kwa

0 comments:

DAVID RUDISHA KUKOSA MASINDANO YA RIADHA NCHINI MOSCOW

epa03353379 David Lekuta Rudisha of Kenya celebrates winning the men's 800m final at the London 2012 Olympic Games Athletics, Track and Field events at the Olympic Stadium, London, Britain, 09 August 2012. At right is Nijel Amos of Botswana who placed second. EPA/BERND THISSEN +++(c) dpa - Bildfunk+++
Zambia, Zimbabwe kumenyana fainali ya Cosafa Jumamosi hii, timu za Ujerumani kujipima nguvu huko mjini Monchengladbach. David Rudhisha kukosa mashindano ya Moscow na timu za Ulaya zaanza kujianda na msimu wa ligi.
Msukosuko klabu bingwa Afrika
Mashindano ya ligi ya vilabu bingwa vya Afrika yamekumbwa na msukosuko mwishoni mwa juma hili huku mechi moja ikifutwa na nyengine ikiwa haijulikani itachezwa lini. Mkasa huo ni wa kundi B, pambano kati ya Coton Sport ya Cameroon na Sewe ya Cote dÍvoire. Pambano hilo sasa limeahirishwa kwa wiki moja pakisubiriwa matokeo ya mazungumzo baina ya chama cha kandanda cha Cameroon na Shirikisho la kandanda la kimataifa FIFA, kuhusu hatua yake ya kupiga marufuku shughuli zote za kandanda katika taifa hilo la Afrika magharibi.
Mchuano wa Coton na Sewe ulikuwa ufanyike Jumamosi hii huko Garoua, lakini Shirikisho la soka barani Afrika CAF limesema huenda sasa zitamenyana Julai 27 ikitarajiwa kwamba FIFA itaondoa amri yake ya kuisimamisaha Cameroon. Shirikisho hilo la soka la kimataifa liliipiga

0 comments:

LIGI KUU YA VODACOM KUWANIA UBINGAWA WA TANZANIA BARA MSIMU WA 2013/2014


Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kuwania ubingwa wa Tanzania Bara msimu wa 2013/2014 inaanza kutimua vumbi Agosti 24 mwaka huu kwa timu zote 14 kuwa viwanjani katika miji saba tofauti.



Hata hivyo, kabla ya ligi hiyo kuanza kutakuwa na mechi ya kufungua msimu (Ngao ya Jamii- Community Shield) kati ya bingwa mtetezi Yanga na Makamu bingwa Azam itakayochezwa Agosti 17 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.



Mechi za VPL za Agosti 14 mwaka huu zitakuwa kati ya Yanga na Ashanti United (Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam), Mtibwa Sugar na Azam (Uwanja wa Manungu, Morogoro), na JKT Oljoro na Coastal Union (Uwanja wa Kumbukumbu ya Sheikh Kaluta Amri Abeid, Arusha).



Nyingine ni Mgambo Shooting na JKT Ruvu (Uwanja wa Mkwakwani, Tanga), Rhino Rangers na Simba (Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi, Tabora), Mbeya City na Kagera Sugar (Uwanja wa Kumbukumbu ya Sokoine, Mbeya), na Ruvu Shooting na Tanzania Prisons (Uwanja wa Mabatini, Mlandizi, Pwani).



Mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo utamalizika Novemba 3 mwaka huu wakati wa pili utamalizika Aprili 27 mwakani.



TAIFA STARS KWENDA KAMPALA J5

Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inaondoka Mwanza keshokutwa (Julai 24 mwaka huu) kwenda Kampala, Uganda kwa ajili ya mechi ya marudiano ya Kombe la CHAN itakayochezwa Jumamosi (Julai 27 mwaka huu) Uwanja wa Mandela kuanzia saa 10 kamili jioni.



Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager iko kambini jijini Mwanza chini ya Kocha Kim Poulsen tangu Julai 14 mwaka huu kujiandaa kwa mechi hiyo itakayoamua ni timu ipi kati ya hizo mbili itacheza Fainali za CHAN zitakazofanyika mwakani nchini Afrika Kusini.



Timu hiyo itaondoka Uwanja wa Ndege wa Mwanza saa 7.25 mchana kwa ndege ya PrecisionAir, na inatarajiwa kutua Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Entebbe saa 10.15 jioni.



Wakati huo huo, Kocha Kim Poulsen kesho (Julai 23 mwaka huu) atakuwa na mkutano na waandishi wa habari kuzungumzia maandalizi ya kikosi chake. Mkutano huo utafanyika saa 5 kamili asubuhi kwenye hoteli ya La Kairo jijini Mwanza.



WAAMUZI WA MCHEZO WA STARS VS UGANDA

Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limeteua waamuzi kutoka Madagascar kuchezesha mechi kati ya Tanzania (Taifa Stars) na Uganda (The Cranes) itakayochezwa Jumamosi (Julai 27 mwaka huu) Uwanja wa Mandela ulioko Namboole nje kidogo ya Jiji la Kampala.



Waamuzi wataongozwa na Kanoso Abdoul Ohabee wakati mwamuzi msaidizi namba moja ni Andirvoavonjy Pierre Jean Eric. Mwamuzi msaidizi namba mbili ni Jinoro Velomanana Ferdinand huku Andriamiharisoa Hubert Marie Bruno akiwa mwamuzi wa mezani (fourth official).



Kamishna wa mechi hiyo ya marudiano ya raundi ya mwisho kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Afrika kwa Wachezaji wa Ndani (CHAN) ni Ismail Kamal kutoka Ethiopia.



Mechi hiyo namba 38 itachezwa kuanzia saa 10 kamili jioni kwa saa za Afrika Mashariki. Taifa Stars ilipoteza mechi ya kwanza iliyochezwa Julai 13 mwaka huu jijini Dar es Salaam kwa bao 1-0.



Taifa Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager iko kambini jijini Mwanza ikijiandaa kwa mechi hiyo itakayoamua ni timu ipi kati ya hizo mbili itacheza Fainali za CHAN mwakani nchini Afrika Kusini.

0 comments:

PAPA FRANCIS AUDHURIA SIKU YA VIJANA DUNIANI NCHINI BRAZIL


Baba mtakatifu Francis amepokewa kwa vifijo na nderemo na maelfu ya waumini wa kanisa katoliki alipowasili nchini Brazil kuhudhuria siku ya vijana duniani, lakini baada ya mapokezi hayo,kulishuhudiwa maandamano
Papa Francis mwenye umri wa miaka 76 alibebwa katika gari lililo wazi na kuzunguka mji mkuu wa Brazil, Rio de Janeiro katika ziara yake ya wiki moja katika nchi hiyo ambayo idadi ya waumini wa kanisa katoliki inazidi kudidimia na hatua zake za kiuchumi zimekubwa na ghasia kutoka kwa umma katika siku za hivi karibuni.
Kiongozi huyo mzaliwa wa Argentina ambaye ndiye wa kwanza kutokea mataifa ya Amerika kusini kuliongoza kanisa hilo, alilakiwa na waumini wake lakini askari wa usalama walitumia mabomu ya kutoa machozi na maji ya kuwatawanya waandamanaji walioanza kurusha mabomu ya petroli baada ya papa kukutana na Rais wa Brazil Dilma Rousef katika ikulu ya gavana wa jimbo hilo.
Papa Francis akiwapungia waumini alipowasili Rio de JaneiroPapa Francis akiwapungia waumini alipowasili Rio de Janeiro
Siku ya vijana duniani yaadhimishwa
Papa Francis yuko nchini Brazil kuhudhuria siku ya vijana duniani,siku ambayo ilianzishwa mwaka 1985 na papa John Paul wa pili.Siku hii inaadhimishwa rasmi hii leo ambapo takriban vijana milioni 1.5 wanatarajiwa kuhudhuria.
Licha ya ulinzi mkali kutokana na ziara hiyo ya papa ambapo wanajeshi 30,000 na mapolisi wanashika doria, watu kadhaa waliweza kufikia gari la papa na hata kumgusa.Papa huyo alisalimiana nao kwa mikono na kuwabusu watoto.
Jeshi lilitangaza Jumapili iliyopita kuwa liligundua bomu wakati wa kikao cha mazoezi katika choo cha kanisa la Our Lady of Aparecida katika jimbo la Sao Paulo ambako kiongozi huyo anatarajiwa kutembelea hapo kesho.
Baba mtakatifu amepata umaarufu sana katika miezi minne tangu kuchaguliwa kuliongoza kanisa katoliki kutokana na unyenyekevu wake na kuwajali maskini.
Vijana wengi hawana ajira
Alipokuwa kwenye ndege kuelekea Rio,papa alilalama kuwa karibu kizazi kizima cha vijana kiko katika hatari ya kutojua ni kipi kitokanacho na kazi kutokana na mzozo wa kiuchumi ambao umewaacha vijana wengi bila ajira katika nchi nyingi za ulaya na kuwaacha nyuma vijana maskini wa kutoka nchi zinazoendelea.
Baba mtakatifu Francis akiwasli BrazilBaba mtakatifu Francis akiwasili Brazil
Serikali ya Brazil imetumia dola milioni 52 kwa ajili ya ziara hiyo ya papa lakini haonekani kulengwa na waandamanaji wa Brazil wanaoghadhabishwa na maamuzi ya kiuchumi ya serikali yao.
Kanisa katoliki linazidi kupoteza umaarufu wake nchini humo kutokana na kuinukukia kwa makanisa ya kiinjili na kuenea kwa maadili ya kilimwengu.
Zaidi ya asilimia 90 ya wabrazil walijitambulisha kuwa wakatoliki miaka ya 70 lakini kura ya maoni iliyotolewa Jumapili iliyopita inaonyesha ni asilimia 57 tu ya wabrazil wanaojiita wakatoliki huku asilimia 28 wakisema ni wapentekosti au waumini wa makanisa ya kiinjili.
Papa Francis anatarajiwa kutembelea mitaa duni mjini Rio na kukutana na wafungwa wa umri mdogo katika hatua ya kuendeleza msingi wake wa wito wa kutaka kuona kanisa nyenyekevu linalojitolea kuwasaidia wasiobahatika katika jamii.

0 comments:

MAMIA YA WAFUNGWA WATOROSHWA NCHINI IRAQ

ATTENTION EDITORS - VISUAL COVERAGE OF SCENES OF INJURY OR DEATH An police officer inspects the site of a bomb attack at a coffee shop in Kirkuk, 250 km (155 miles) north of Baghdad, July 12, 2013. A bomb attack in a cafe in northern Iraq killed at least 31 people on Friday, police and medics said. The blast took place in the ethnically mixed city of Kirkuk, in a coffee shop where people had gathered after breaking their fast for the Muslim holy month of Ramadan. REUTERS/Ako Rasheed (IRAQ - Tags: CIVIL UNREST POLITICS) TEMPLATE OUT - eingestellt von gri
Wanamgambo wenye silaha nchini Iraq wamevamia magereza mawili, likiwemo lile maarufu la Abu Ghraibu, na kuanzisha mapigano yaliyouwa watu 41 na kuwatorosha wafungwa wasiopungua 500.
Mashambulizi hayo ya kupangwa dhidi ya gereza la Taji kaskazini mwa Baghdad na Abu Ghraibu lililoko magharibi mwa mji huo mkuu yalifanywa usiku wa kuamkia leo na yaliendelea

0 comments:

TSVANGIRAI AANDAMWA NA KASHFA HUKU UCHAGUZI UKIKARIBIA

Morgan Tsvangirai, waziri mkuu wa Zimbabwe anayeandamwa na kashfa za kimapenzi
Kituo cha Televisheni cha taifa cha Zimbabwe kimeanzisha kampeni ya kumchafulia jina Morgan Tsvangirai, mpinzani wa rais Robert Mugabe katika uchaguzi mkuu wa tarehe 31,Julai, 2013, na tayari athari zimeanza kuonekana.
Katika matangazo yanayorushwa na kituo hicho cha televisheni ya taifa, kituo hicho kinawaonyesha wapenzi wa zamani wa Morgan Tsvangirai, wakisimulia jinsi alivyowatelekeza. Baada ya simulizi zao huingia maafisa wa chama cha ZANU-PF cha Rais Robert Mugabe, wakiwahimiza wapiga kura kuepuka kumchagua Tsvangirai, ambaye ni waziri mkuu katika serikali ya mpito, wakisema hafai kuliongoza taifa.
Ingawa yapo maswali kadhaa juu ya lugha na mtindo vinavyotumiwa katika matangazo hayo yanayomlenga Tsvangirai, hususan kwa kuzingatia kuwa Zimbabwe ni nchi inayodai kuzingatia maadili, tayari athari zake zimeanza kuonekana. Hata wale watu ambao siku z

0 comments:

CHINA IMELETA BIDHAA, BARABARA, SASA AFRICA YATAKA AJIRA

Chinese woman stand in front of a billboard which promotes the upcoming China-Africa summit meeting, outside a hotel in Beijing Thursday Oct. 26, 2006. Beijing is making unusually lavish efforts to welcome leaders and officials from 48 African nations this week for a landmark summit meant to highlight China's huge and growing role in Africa. The Chinese characters at left read Africa. (AP Photo/Greg Baker)
Licha ya China kuleta bidhaa za bei nafuu, barabara na hata shule barani Afrika, serikali za bara hilo zinaishinikiza nchi hiyo itoe kile Waafrika wengi wanachokihitaji: Ajira.
Ripoti ya hivi karibuni iliyotolewa na tume ya uchumi ya Umoja wa Mataifa kuhusu Afrika UNECA, ilibainisha hatari kuwa uhusiano wa bara hilo na taifa la China lenye uchumi wa pili kwa ukubwa duniani, unaweza kukwaza juhudi la bara hilo kukuza sekta ya viwanda. Biashara kati ya China na Afrika iliongezeka kutoka dola bilioni 10 mwaka 2000, hadi kufikia takribani dola bilioni 200 mwaka huu - miaka minne baada ya nchi hiyo kuipiku Marekani kama mshirika nambari

0 comments:

HIVI NDIVYO MAUAJI YALIVYOFANYIKA HUKO DARFUR KUFATIA KUUWA KWA WANAJESHI 7 WA TANZANIA

Imefahamika kuwa kuuawa kwa wanajeshi saba wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) waliokuwa kwenye operesheni za Jeshi la Kulinda Amani la Umoja wa Mataifa (Unamid), katika Jimbo la Darfur nchini Sudan, kulitokana na shambulio la kushtukiza (Ambush), lililopangwa na waliowashambulia.


Hayo yalielezwa jana jijini Dar es Salaam na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini, Jenerali Davis Mwamunyange, katika salama zake alizozitoa kwa Rais na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Dk. Jakaya Kikwete na waalikwa mbalimbali waliokuwa wamefika kwenye hafla ya kuwaaga mashujaa hao.


Jenerali Mwamunyange alisema wanajeshi hao waliuawa wakati wakisafiri kutoka eneo la Khor Abeche kwenda Nyala wakisindikiza msafara wa waangalizi wa amani wa Umoja wa Mataifa (UN).

“Ilikuwa ni Julai 13, saa tatu asubuhi na walipokuwa wamesafiri umbali wa kilometa 25, walifika kwenye eneo lililokuwa na mteremko mkali na lenye utelezi kufuatia mvua kubwa iliyokuwa imenyesha. Ilibidi wapunguze mwendo wa magari yao ili yaende taratibu, kumbe ndiyo walikuwa wanaingia kwenye ‘ambush’ na kujikuta wakishambuliwa,” alisema.

Alisema kutokana na hali hiyo, ilibidi wapigane kwa weledi mkubwa kwa karibu saa mbili ili kujinasua toka kwenye ambush hiyo, hadi pale walipopata msaada kutoka kwa askari wenzao waliokuja kuwasaidia.

Alisema kutokana na juhudi za kupigana kwa weledi kwa lengo la kujinasua, ilibidi waasi wakimbie, lakini tayari wakiwa wameshaua mashujaa hao saba na kujeruhi wanajeshi wengine 14, kati yao akiwamo ofisa mmoja wa polisi.

HALI ILIVYOKUWA
Shughuli ya kuaga miili ya mashujaa hao saba, Sajini Shaibu Othman, Koplo Oswald Chaula, Koplo Mohamed Ally, Koplo Mohamed Chikilizo, Private Fortunatus Msofe, Private Rodney Ndunguru na Private Peter Werema, ilianza saa tatu asubuhi kwa kuwasili wageni mbalimbali, wakiwamo mawaziri, mabalozi wanaowakilisha nchi zao na maofisa wa UN, maofisa waandamizi wa serikali, wakuu wa majeshi wastaafu na wanadhimu wastaafu.

Pia walihudhuria majenerali wastaafu, majenerali walio kwenye utumishi, wafanyabiashara, akiwamo Dk. Reginald Mengi, familia za wafiwa na wananchi wa kada zote.

VIONGOZI WA KITAIFA WAWASILI
Majira ya saa nne asubuhi, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi aliwasili, akifuatiwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Mohammed Gharib Bilal aliyewasili saa 4:52.

KIKWETE AWASILI
Rais Jakaya Kikwete aliwasili saa 5:08 asubuhi na shughuli ya kuileta miili ya mashujaa kwenye viwanja hivyo vya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Upanga, jijini Dar es salaam ilifuata.

MIILI YAWASILI
Lilianza gari lenye namba 5914 JW 12 lililokuwa limebeba jeneza la Sajini Othman, ambalo lilingia majira ya saa tano na robo asubuhi.

Jeneza hilo lilishushwa na askari wanane wenye vyeo vya sajini wakisindikizwa na askari wawili na kisha kupeleka jeneza hilo, juu ya meza moja maalumu iliyokuwa imeandaliwa.

Hatimaye lilifuata gari namba 5980 JW12 lililokuwa na jeneza la mwili wa Koplo Chaula, lililoingia saa 5:19, kisha gari namba 5907 JW12 lililokuwa na mwili wa Koplo Chikilizo, lililoingia saa 5:23 na gari namba 5913 JW12 lililioingia saa 5: 27, likiwa na mwili wa koplo Ally.

Baadaye lilifuata gari namba 5912 JW12 lililoingia saa 5: 32, likiwa na mwili wa Private Msofe, kisha gari namba 5976 JW12 lililoingia saa 5:36, likiwa na mwili wa Private Ndunguru na mwisho gari namba 5906 JW 12, likiwa na mwili wa Private Werema.

AMIRI JESHI AONGOZA
Rais Kikwete aliongoza waomboleza wote kuaga miili hiyo mnamo saa 5:47 pale alipopita mbele ya majeneza yaliyokuwa yamefunikwa kwa bendera ya taifa na kisha akamalizia kwa kuwapa mkono wa pole familia za wafiwa.

Baadaye Makamu wa Rais, Dk. Bilal alifuata akiwaongoza viongozi mbalimbali waliokuwa kwenye turubai kuu, wakiwamo mawaziri, mabalozi, maofisa wa UN, maofisa waandamizi wa serikali, majenerali wastaafu na maofisa wakuu walioko jeshini.

RISALA ZA RAMBIRAMBI
Zilisomwa rambirambi zilizotumwa kwa mkuu wa majeshi kutoka sehemu mbalimbali, zikiwamo toka kwa mabalozi, maofisa wastaafu, wanajeshi wenzao walio Unamid-Sudan na Jumuiya wa Watanzania wanaoishi Sudan. Aidha, Jumuiya ya Watanzania waishio nchini Sudan walitoa Dola za Marekani 700 kama rambirambi na wanajeshi wenzao walitoa Dola 1,800 kwa marehemu wote.

UN YATOA NISHANI
Katika kutambua mchango wa wanajeshi hao, UN ilitoa medali kwa kila mwanajeshi aliyefariki ambazo kwa mujibu wa Msemaji wa shughuli hiyo ya jana, Kanali Dominick Mrope, zitafikishwa kwa wanaostahili, kwa mujibu wa taratibu za kijeshi.

Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Ali Mohamed Shein, alituma rambirambi kwa mkuu wa majeshi na katika salamu zake zilizosomwa kwa niaba yake na Kamanda wa Kamandi ya Nchi Kavu, Meja Jenerali Mustapha Kijuu, alisikitikia mauaji yaliyofanywa dhidi ya mashujaa hao.

“Natoa salamu zangu kwako mkuu wa majeshi na kwa familia za wafiwa, kufuatia msiba huu mkubwa wa kitaifa. Naomba tuwe na subira na nawatakia nafuu ya haraka, majeruhi wote walioko hospitalini,” alisema.

JK ANENA
Kwa upande wake, Rais Kikwete alisema kwamba atahakikisha anatumia ushawishi wake wote ili kuzishawishi mamlaka za UN na Umoja wa Afrika (AU) zinazosimamia operesheni za amani Darfur, ili ziweze kuruhusu vikosi vinavyoshiriki katika operesheni hizo, kuwa na silaha nzito kwa minajili ya kujilinda kwa mapigo mazito, pale zinaposhambuliwa.

“Nilisikitika sana pale nilipopata habari ya kuuawa kwa mashujaa wetu. Nilijiuliza kwamba, kwa nini watu wa Darfur wawaue wanajeshi wetu walioenda kuwasaidia wapate amani, waendeshe maisha yao katika hali ya utulivu. Ndiyo maana niliongea na Rais Omar al Bashir, ahakikishe wanawatafuta wahalifu hawa haraka na kuwafikisha mbele ya vyombo vya sheria,” alisema.

Hata hivyo, Rais aliwaasa Watanzania na wanajeshi kwa ujumla kutokatishwa tamaa na kilichotokea, bali wachukue kama changamoto ya kujiimarisha zaidi.

Aliwakumbusha Watanzania kuwa toka uhuru, Tanzania imekuwa na falsafa ya kusaidia mataifa mbalimbali kwa njia za kidplomasia na kivita, ili yapate amani kama ilivyofanyilka katika nchi za Msumbiji, Liberia, Sierra Leone, Eritrea, Lebanon, Sudan na sasa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

Alisema tokea Tanzania ianze kuchangia wanajeshi wake kule Sudan, mwaka 2007, JWTZ imefanya kazi zake kwa weledi na umakini wa hali ya juu, kiasi

0 comments:

SAKATA LA USAJILI WA CESC FABREGAS: ARSENAL HAWATOPATA CHOCHOTE KWENYE ADA YA UHAMISHO? ISIPOKUWA TU PALE ITAPOPATIKANA FAIDA YA MAUZO YA MCHEZAJI HUYO.

Ripoti kwamba Arsenal wana haki ya kupata 50% ya fedha za ada ya uhamisho ikiwa Cesc Fabregas atahama kutoka Barcelona kwenda Manchester United sio za kweli kabisa, kwa mujibu wa ESPN.
Leo Jumatatu, David Moyes amethibitisha United imetuma ofa ya pili ambayo inadhaniwa kuwa ni £30 million kwa ajili ya kumsaini mchezaji huo wa zamani wa Arsenal, na sasa wanasubiri majibu kutoka kwa mabingwa hao wa Spain.

Huku sasa tayari kukiwa na ofa rasmi mezani, Barcelona wanapaswa kuwataarifu Arsenal na kuwapa nafasi ya kumsajili tena mchezaji huyo kwa bei watakayokubaliana.

The Gunners wana haki ya kumsaini tena Fabregas kwa ada ambayo ipo karibu na waliyotoa United.
Ikiwa watashindwa kufanya hivyo, watapokea 50% ya faida yoyote ambayo FC Barcelona watapokea ikiwa watamuuza Fabregas kwa klabu nyingine. Na kwa ada ya uhamisho wa £30million ni vigumu kwa Arsenal kupata chochote

0 comments:

ANGALIA PICHA ZA RAIS KIKWETE AKIONGOZA MAZISHI YA WANAJESHI WALIOUAWA DARFUR

Miili ya Mashujaa wetu iliwasili eneo la tukio tayari kwa maagano




Rais Kikwete na Mkewe Mama Salma waliongoza

0 comments:

HUYU NDO MMILIKI WA HOME SHOPPING CENTRE ALIYEMWAGIWA TINDIKALI

MSHTUKO mkubwa ulijiri Jumamosi iliyopita, ikiwa ni baada ya kusambaa kwa habari za kumwagiwa tindikali, mfanyabiashara mwenye ‘levo’ ya ubilionea, Said Said Mohammed, 42, ambaye ndiye mmiliki na Mkurugenzi Mkuu wa Home Shopping Centre.

Said ambaye kwa utambulisho mwingine anajulikana kama Said Mohammed Saad, alimwagiwa tindikali Ijumaa iliyopita, saa 2 usiku, lakini habari zake zikavuma Jumamosi, hivyo kuibua taharuki ya aina yake.

Kuhusu nani alimmwagia tindikali hiyo, sababu ya kutendwa unyama huo, yupi mhusika mkuu wa ukatili wenyewe na malengo ya uharamia, kwa jumla, hayo ni maswali yanayoendelea kuitesa familia yake, watu wa karibu pamoja na Jeshi la Polisi Tanzania.

Taarifa za kipolisi zinathibitisha kwamba alimwagiwa tindikali

0 comments:

AGNESS MASOGANGE ATAPANDISHWA KIZIMBANI TENA TAREHE 13 AGOSTI MWAKA HUU

Hatima ya msanii anayeshiriki katika video za wasanii wa muziki wa bongo fleva, Agnes Jerald 'Masogange' na mwenzake Melisa Edward, waliokamatwa Afrika Kusini na dawa za kulevya kesi yao inatarajiwa kusomwa tena tarehe 13 Agosti mwaka huu nchini humo.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, Kamanda wa Polisi wa Kikosi cha Kudhibiti Dawa za Kulevya Tanzania, Godfrey Nzowa aliweka wazi kuwa wanadada hao wawili tayari walishapandishwa kizimbani wiki iliyopita.

Alisema kuwa kutokana na ushahidi kutokukamilika ndiyo sababu ya akinadada hao kusubiri kupanda kizimbani tena tarehe 13 ya mwezi ujao.

Kamanda Nzowa aliweka wazi kuwa nchi zote mbili zinashirikiana kwa ajili ya kufanya upelelezi wa jambo hilo: "Nchi zote mbili tunategemeana kwa upelelezi, hivyo sisi huku tunafanya wa kwetu na wao wanafanya wa kwao mwishoni tunaulizana tulipofikia hivyo ndivyo tunavyofanya kazi

0 comments:

POLISI MKOANI MWANZA YAFAFANUA KWA KINA KUHUSU VIELELEZO VYA KESI VILIVYOIBIWA KITUONI HAPO


WATU wasiofahamika idadi yao wanaodhaniwa wezi, wameiba vielelezo katika stoo ndogo ya Kituo Kikuu cha Polisi Kati, Wilaya ya Nyamagana, mkoani Mwanza baada ya kuvunja madirisha.

Tukio la wizi huo lilifanyika Julai 15, mwaka huu, majira ya usiku wa kuamkia Jumatano katika jengo la Polisi Wilaya ya Nyamagana.

Akizungumza na gazeti la MAJIRA jana, Kamanda wa Polisi Mkoa Naibu Kamishna wa Polisi (DCP) Ernest Mangu, alisema wezi hao kabla ya kuingia ndani ya jengo hilo, walivunja dirisha la ofisi za Elimu, Ukaguzi Kanda ya Ziwa na walipofanikiwa kuingia ndani, walivunja dirisha na kuingia kwenye ofisi za Polisi Nyamagana na kutanua nondo kwa jeki na kisha kuingia kwenye stoo ndogo ambamo vielelezo hivyo vilitunzwa na kuiba begi moja la nguo na kompyuta mbili mpakato.

Moja ya kompyuta hizo ni kielelezo katika kesi ya ujambazi ambayo mtuhumiwa alikamatwa nayo, ambaye kwa sasa yuko mahabusu katika Gereza Kuu la Butimba.

Kamanda Mangu alisema kompyuta ya pili ni kielelezo cha kesi ya uharibifu wa mali inayomkabili fundi mmoja na begi la nguo

0 comments:

WALIOWAUA WANAJESHI WA TANZANIA WATAJWA.....NI KUNDI LA "JANJAWEED" LINALOUNGWA MKONO NA SERIKALI YA SUDAN


WAKATI miili ya wanajeshi saba ikiwa imeagwa jana katika Viwanja vya Makao Makuu ya Jeshi la Wananchi wa Tanzania, imeelezwa kuwa kundi la Janjaweed linaloungwa mkono na serikali ya Sudan ndilo lililowavamia na kuwaua askari hao nchini humo na kuwajeruhi wengine 17 .

Wanajeshi hao wa Tanzania ambao walikuwa ni sehemu ya Jeshi la Kulinda Amani la Umoja wa Mataifa (Unamid), walifanyiwa unyama huo

0 comments:

MR. NICE APATA SHAVU JINGINE NCHINI KENYA BAADA YA KUTEMWA NA GRANDPA


Ikiwa ni zaidi ya mwezi mmoja toka staa wa Bongo Luca Mkenda aka Mr Nice apoteze nafasi ya kufanya kazi na label ya GrandPa ya Kenya kwa shutuma za uvivu, kushindwa kutoa ushirikiano na ukiukaji wa mkataba hatimaye mlango mwingine umefunguka kwa nyota huyo wa ‘Kikulacho’.


Mr Nice ambaye bado yuko Kenya anatarajia kujiunga na label nyingine nchini humo ‘Candy Records’ ambayo ina miezi michache toka ianzishwe. 


Kwa mujibu wa CEO wa label hiyo John Kariuki aliyekuwa

0 comments:

SERIKALI YASISITIZA KUWA "KODI YA LINE ZA SIMU" IKO PALE PALE


Waziri wa Fedha, William Mgimwa, amesisitiza uamuzi wa Serikali kuendelea kutoza Sh 1,000 kwa kila mwezi kwa laini ya simu, licha ya kampuni za simu na wanasiasa kupinga.

Akizungumza na mwandishi juzi, Mgimwa alikumbusha wanaolalamikia kodi hiyo, kwamba suala la ulipaji kodi kwa taasisi au watu binafsi, ni la kisheria kulingana na mapato yao na hali halisi iliyopo.
 

Pia alieleza kushangazwa na matangazo ya baadhi ya kampuni kuhusu utozwaji kodi wananchi akisema wananchi ndio wanataka barabara, maji na umeme vijijini na kodi hizo zinakwenda kutumika huko.

0 comments:

CHADEMA YAJITOA KUWANIA UMEYA WA ARUSHA BAADA YA KUMUOMBA MEYA GAUDENCE KUTENDA HAKI


Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimeamua kuachana na kuwania umeya wa Jiji na badala yake kimemwomba Meya, Gaudence Lyimo (CCM), atende haki.

Katibu wa Kanda ya Kaskazini wa chama hicho, Amani  Golugwa

0 comments:

WEMA SEPETU APANDISHWA KIZIMBANI KWA MARA YA KWANZA BAADA YA KUMTUKANA MENEJA WA HOTELI

KUNA kila dalili kwamba mrembo anayetamba kwenye filamu za Kibongo, Wema Isaac Sepetu   jela inamwita na anatakiwa kufanya maombi ili kukwepa kifungo maishani mwake.

Hali hiyo inafuatia staa huyo kupandishwa kizimbani kwa mara nyingine tena Jumatano iliyopita, pale alipopanda katika Mahakama ya Mwanzo ya Kawe jijini Dar kwa kosa la kumpiga na kumtukana matusi ya nguoni meneja wa

0 comments:

VODACOM WAZINDUA CHARGER YA SIMU INAYOTUMIA MIONZI YA JUA

Vodacom Tanzania sasa wanauza charger za simu zinazojulikana kama ReadySet Charge ambazo zinatumia njia mbadala ya chanzo cha nishati …

Charger hizo zinazotumia mionzi ya jua zinawafaa wafanyabishara

0 comments:

"NIPO TAYARI KUPIGANA NA JACK WOLPER ENDAPO ATAENDELEA KULITUMIA JINA LANGU KUJIPATIA UMAARUFU"...BABY MADAHA


Staa wa muziki na filamu Bongo, Baby Joseph ‘Baby Madaha’ ameomba pambano la ngumi dhidi ya Jacqueline Wolper ili waweze kumaliza ubishi wa bifu lao.


Akipiongea na mwandishi wetu, Baby alisema,
amechoshwa kusikia tambo za mpinzani wake huyo hivyo kama kweli ni mwanamke, wakutane kwa ngumi ili amuoneshe cha mtema kuni.



“Asiniambie mimi natafuta kiki, mimi ni msomi kuliko

0 comments:

CCM NAYO YAPINGA KODI YA LINE ZA SIMU YAIATAKA SERIKALI KUTAFUTA NJIA NYINGINE


CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimekuja juu na kuitaka Serikali kuangalia njia nyingine mbadala ya kukusanya kodi na kuachana na mpango wa kuanza kuwatoza wananchi tozo ya Sh 1,000 kila mwezi kwa kila laini ya simu ya kiganjani.

Hatua hiyo, inatokana na kilio cha, wananchi ambao tangu Bunge la Bajeti kwa mwaka 2013/14 kupitisha sheria hiyo, kumekuwa na manung’uniko mengi.

Uamuzi huo, ulipitishwa na Bunge baada ya mjadala mkali pindi bajeti

0 comments:

MATUKIO MUHIMU KATIKA MIAKA 50 YA UMOJA WA MATAIFA

Burundische Soldaten bei der Beerdigung des Präsidenten Melchior Ndadaye, der bei einem Putsch 1993 ums Leben kam ALEXANDER JOE/AFP/Getty Images


Matukio muhimu katika miaka 50 ya Umoja wa Afrika

Majeshi yasiyopendwa

Mwanzoni mwa miaka ya 1990, OAU ilikuja na sera mpya: Afrika

0 comments:

KERRY AITAKA DUNIA KUCHUKUA HATUA JUU YA SYRIA

US Secretary of State John Kerry speaks during a joint press conference as Jordan's Foreign Minister Nasser Judehlooks on, on July 17, 2013 at the Ministry of Foreign Affairs in Amman. Kerry met with Arab League officials to discuss his push to thaw out the frozen peace process, as Palestinians said there had been progress. AFP PHOTO/Mandel NGAN-POOL (Photo credit should read MANDEL NGAN/AFP/Getty Images)
Waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani John Kerry ametoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kuchukua jukumu kubwa zaidi katika kuuangalia mzozo wa kibinadamu nchini Syria kutokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo.
Kerry ameyasema hayo baada ya kutembelea kambi ya wakimbizi wa Syria nchini Jordan.

0 comments:

UMOJA MATAIFA WAPELEKA MAJESHI NCHINI CONGO

Congolese Army soldiers man a foward position in Kanyarucinya, some 12 kms from Goma, in the east of the Democratic Republic of the Congo on July 16, 2013. The army in the Democratic Republic of Congo on July 16 pursued an offensive against rebels of the M23 movement to protect the North Kivu provincial capital of Goma. M23, a movement launched by Tutsi defectors from the army who accuse the Kinshasa government of reneging on a 2009 peace deal, last year occupied Goma for 10 days before pulling out under international pressure. AFP PHOTO / PHIL MOORE (Photo credit should read PHIL MOORE/AFP/Getty Images)
Umoja wa Mataifa umesema upo tayari kupeleka jeshi katika uwanja wa mapambano huko mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo kukabiliana na Waasi. Hatua inayotokana na malalamiko ya waandamanaji mjini Goma.
Waandamanaji wanalalamika kwamba walinzi wa amani wamekuwa dhaifu katika kukabiliana na vitendo vya waasi katika maeneo hayo.
Jeshi la Umoja wa Mataifa nchini Kongo limeonekana kujiweka kando kabisa wakati wapiganaji waasi wa kundi la M23 likifanya mashambulizi dhidi ya majeshi ya serikali katika eneo kubwa la mashariki la mji wa Goma.
Msemaji wa Umoja wa Mataifa Martin Nersirky amenukuliwa na shirika la habari la Ufaransa, AFP akisema jeshi la ulinzi wa amani nchini Kongo, MONUSCO kwa wakati wote katika operesheni zake nchini humo halijajiingiza katika uhasama.
Jeshi lipo katika hali ya tahadhari
A Congolese army soldier walks through the bush, back from an attack position north-west of Munigi, overlooking the front-line, in the east of the Democratic Republic of the Congo on July 15, 2013. Fighting broke out yesterday between M23 rebels and the national army, and continued today, with heavy artillery fire north-west of Munigi and the army claiming to have taken ground. AFP PHOTO/PHIL MOORE (Photo credit should read PHIL MOORE/AFP/Getty Images) Mwanajeshi wa Kongo kwenye doria katika viunga vya Goma
Msemaji huyo ameongeza kusema majeshi ya bado yapo katika hali ya tahadhari na kujitayarisha kujiingiza katika mapigano hayo, kwa kujumuisha jeshi jipya kwa lililopo nchini humo kwa hivi sasa kwa ajili ya kuleta ustawi. Amesema operesheni hiyo inaweza kuwaweka katika hali ya wasiwasi wakazi wa eneo hilo la mashariki ya Kongo, na hasa Goma.
Kwa mujibu wa AFP, tangu jana kumekuwa kimya katika eneo la Goma. Lakini kulikuwa na maandamano katika mji huo, ambapo baadhi ya wamelituhumu jeshi hilo la Umoja wa Matiafa kwa kutotoa ushirikiano wa kutosha kwa majeshi ya serikali ya Kongo.
Doria yaendelea Goma
Hadi sasa kuna wanajeshi 2,000 kutoka Afrika Kusini, kati ya 3,000 wanaounda jeshi hilo la Umoja wa Mataifa. Idadi iliyobaki kati ya hao inatoka Tanzania na Malawi. Majeshi hayo yanafanya tu, doria na kwamba mpaka sasa hawajafanya shambulizi lolote pamoja na kuwa na mamlaka ya kufanya hivyo kama inavyoelekeza mamlaka waliopewa na baraza la usalama la Umoja wa Mataifa.
Msemaji wa Umoja huo Nesirky amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amesikitishwa sana uhasama mpya katika maeneo ya mji mkuu wa Kivu ya Kaskazini. Kiongozi huyo wa ametaka pande zote husika katika eneo hilo kufanya jithada katika kudhibiti kuongeka kwa mogogoro huo ambao utazidisha matatizo kwa wakazi.
Waasi wa M23 walifanya mashambulizi Jumapili iliyopita ambapo Jeshi la Kongo lilisema kiasi ya watu 130, waliuwawa.

0 comments:

MAANDAMANO MENGINE MAKUBWA YAANZA KUFANYIKA MISRI

 Supporters of deposed Egyptian President Mohamed Mursi hold posters during a protest outside Rabaa Adawiya mosque in Cairo July 9, 2013. Egypt's interim President Adli Mansour on Tuesday named liberal economist and former finance minister Hazem el-Beblawi as prime minister in a transitional government, as the authorities sought to steer the country to new parliamentary and presidential elections. The posters read, No substitute for the legitimacy. REUTERS/Louafi Larbi (EGYPT - Tags: POLITICS CIVIL UNREST)
Jeshi la Misri limeimarisha ulinzi kwenye majengo ya serikali katika siku ambayo kundi la Udugu wa Kiislamu na wapinzani wao wamepanga maandamano makubwa kutetea misimamo yao juu ya kupinduliwa kwa Mohamed Mursi.
Wanajeshi wanaripotiwa kuweka vizuizi kwenye barabara zote muhimu kuelekea mji mkuu, Cairo, ambako ndiko kitovu cha maandamano ya makundi mawili yanayopingana nchini Misri.
Jeshi limesema linajaribu kuzuia kuingizwa kwa silaha na sio kuzuwia

0 comments:

JANGA LA KITAIFA SHULE KUKOSA WANAFUNZI

 
Jambo ambalo hakulitaja pengine kwa makusudi au kwa bahati mbaya ni ukweli kwamba upungufu wa wanafunzi wa kujiunga na kidato cha tano mwaka huu utakuwa mkubwa zaidi kwa kuwa zaidi ya robo ya wanafunzi waliochaguliwa kuingia katika sekondari na vyuo vya Serikali watajiunga na sekondari za watu binafsi.
Takwimu zilizotolewa juzi na Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kuhusu wanafunzi waliochaguliwa kujiunga na kidato cha tano katika sekondari za Serikali na vyuo vya ualimu mwaka huu zinasononesha na zimethibitisha pasipo kuacha shaka kwamba nchi yetu inaelekea kuzimu katika suala zima la elimu.
   Hatuhitaji kupiga ramli kujua kwamba Serikali isipochukua hatua stahiki haraka iwezekanavyo, hata mafanikio kiduchu tuliyokwisha kuyapata yatapotea na kuiacha sekta nzima ya elimu ikiwa mfu. Tunasema hivyo kutokana na takwimu za kutisha zilizotangazwa na wizara hiyo juzi kuonyesha kwamba kutakuwa na upungufu wa wanafunzi 10,074 wa kidato cha tano katika sekondari zinazomilikiwa na Serikali.
   Picha halisi ni mbaya zaidi kuliko ile iliyoonyeshwa na Naibu Waziri wa wizara hiyo, Philipo Mulugo wakati alipotangaza uteuzi wa wanafunzi hao katika mkutano wake na waandishi wa habari juzi. Jambo ambalo hakulitaja pengine kwa makusudi au kwa bahati mbaya ni ukweli kwamba upungufu wa wanafunzi wa kujiunga na kidato cha tano mwaka huu utakuwa mkubwa zaidi kwa kuwa zaidi ya robo ya wanafunzi waliochaguliwa kuingia katika sekondari na vyuo vya Serikali watajiunga na sekondari za watu binafsi. Hivyo, hapa tunazungumzia upungufu wa wanafunzi wapatao 13,000 hivi.
   Kwa hiyo, tunaishauri Serikali ilione  tatizo hilo katika mapana yake, kwa maana ya kuliona kama janga la kitaifa na kulifanya kipaumbele cha kwanza katika mipango ya maendeleo. Elimu ni suala mtambuka kwa sababu inagusa kila sekta, zikiwamo nishati, maji, miundombinu na kilimo ambazo zimetajwa kuwa vipaumbele vya Serikali katika mwaka huu wa fedha. Ndiyo maana tunasema fedha zinazotengwa kila mwaka kwa ajili ya elimu zisipungue asilimia 30 ya bajeti ya Serikali na hili linawezekana iwapo tu tutapunguza vipaumbele ili mkazo  uwekwe kwenye elimu.
   Lazima tufike mahali tukiri kwamba moja ya changamoto kubwa zinazotukabili kama taifa ni kushuka kwa viwango vya elimu kwa kasi ya kutisha. Takwimu zilizotolewa na

0 comments:

''SIWEZI KUMUOMBA MSAMAHA DIAMOND KWENYE TWITTER''.... PREZZO


Rapcellency, Prezzo amesema hawezi kumuomba msamaha Diamond kwenye Twitter kwakuwa anaamini hakuna alichomkosea na ni jambo la kitoto.
Akiongea jana  mchana kwenye kipindi cha Mambo Mseto cha Radio Citizen, kinachoendeshwa Mzazi Willy M. Tuva, Prezzo amesema Diamond ndiye aliyemchokoza baada ya wasanii hao kutumbuiza mwanzoni mwa mwezi huu kwenye tamasha la Matumaini.
  Prezzo anadai aligundua kuwa Diamond alimponda kwenye

0 comments:

GAY NA POWELL KUTOSHIRIKI MASHINDANO YA DUNIA MOSCOW

 epa03775607 Tyson Gay from the USA celebrates after winning the mens 100 m race at the Athletissima IAAF Diamond League athletics meeting in the Stade Olympique de la Pontaise in Lausanne, Switzerland, 04 July 2013. EPA/JEAN-CHRISTOPHE BOTT +++(c) dpa - Bildfunk+++
Shirikisho la mchezo wa riadha duniani lasema mfumo wake wa kupambana na wanariadha wanaotumia madawa ya kuongeza nguvu unafanyakazi, wakimbiaji mashuhuri Tyson Gay na Asafa Powell wanasa katika mtego,wa Doping.
Shirikisho la mchezo wa riadha ulimwenguni IAAF limesema kuwa kuaminika kwa mpango wake wa kupambana na wanariadha wanatumia madawa ya kutunisha misuli kumeimarika na sio kuporomoka baada ya wakimbiaji nyota Asafa Powell na Tyson Gay wa Marekani kunasa katika mtego huo baada ya kupatikana na hatia ya kutumia madawa ya kuongeza nguvu, ambayo yamepigwa marufuku.
Gay , bingwa wa zamani wa dunia ambaye alishinda mbio za mita 100, na 200 katika mashindano ya kitaifa nchini Marekani mwezi uliopita, amesema kuwa atajitoa katika mashindano yajayo ya ubingwa wa dunia nchini Urusi mwezi ujao.
(FILE) A file picture dated 30 August 2007 shows Tyson Gay of the USA celebrating after winning the 200m final at the 11th IAAF World Championships in Athletics, Osaka, Japan. Tyson is awarded the 2007 Male World Athlete of the Year during the celebrations of the World Athletics Gala hosted by International Athletic Foundation (IAF) Honorary President HSH Prince Albert II of Monaco and IAF & IAAF President Lamine Diack in the Salle des Etoiles of the Sporting Club dÒEt- Monte Carlo, 25 November 2007. EPA/KIMIMASA MAYAMA +++(c) dpa - Bildfunk+++
Bingwa wa zamani wa mbio za mita 100 na 200 duniani Tyson Gay
Wakabiliwa na adhabu
Powell ambaye alishikilia rekodi ya dunia katika mbio za mita 100 hadi Usain Bolt alipoishusha mwaka 2008, pamoja na bingwa wa medali ya dhahabu katika mashindano ya Olimpiki Sherone Simpson pia wanakabiliwa ya hatua ya kuzuiwa kushiriki michezo ya riadha baada ya

0 comments:

MATUKIO MUHIMU KATIKA MIAKA 50 YA UMOJA WA AFRICA

  • Westsaharische Frauen in einem Flüchtlingscamp (c) dpa - Bildfunk+++

    Matukio muhimu katika miaka 50 ya Umoja wa Afrika

    Sera ya ukombozi wa kijeshi

    Licha ya kanuni zake kwamba hali ya mipaka inabaki bila kuguswa, OAU iliitambua Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kiarabu ya Sahara (Sahara Magharibi), iliyotangazwa na Chama cha Polisario. Hii ilipelekea nchi ya Morokko kujitoa katika umoja huo, na hadi wakati huu, imeendelea kuwa nchi pekee ya kiafrika iliyojitoa katika umoja huo kwa hiari.CHANZO DW

0 comments:

MGOMO WA MASAA 24 WAIPOOZESHA UGIRIKI,BUNGE LACHEMSHA LAJIANDAA KUPITISHA MPANGO UNAOPIGWA

 Anti-austerity protesters and parliamentarians of the anti-bailout radical leftist SYRIZA party participate in a rally in Athens, July, 16, 2013, during a 24-hour general strike. Trains ground to a halt and hospitals worked with emergency staff as Greek workers went on strike on Tuesday in protest at government plans to fire thousands of public sector employees. REUTERS/John Kolesidis (GREECE - Tags: POLITICS BUSINESS CIVIL UNREST)
Mgomo wa saa 24 wa wafanyakazi wa sekta ya umma nchini Ugiriki umeipoozesha kabisa nchi hiyo, huku bunge likitarajiwa hivi leo kupitisha mpango unaopingwa na wafanyakazi hao wa kukata nafasi za ajira kwenye serikalini.
Maelfu ya wafanyakazi wenye hasira waliacha ofisi zao na kuandamana mbele ya bunge la Ugiriki hapo jana, dhidi ya mpango wa serikali kuwapunguza wafanyakazi wa sekta ya umma, ili kukidhi matakwa ya wakopeshaji wa kigeni.
Mgomo huo dhidi ya mpango mpya wa kuwahamisha au kuwafukuza kaz

0 comments:

BARAZA LA USALAMA LA UMOJA WA MATAIFA RWANDA LAHITUHUMU CONGO KUSHIRIKIANA NA WAASI

 Rwanda's President Paul Kagame attends the signing ceremony of the Peace, Security and Cooperation Framework for the Democratic Republic of Congo and the Great Lakes, at the African Union headquarters in Ethiopia's capital Addis Ababa Feburary 24, 2013. A U.N .-mediated peace deal aimed at ending two decades of conflict in the east of the Democratic Republic of Congo was signed on Sunday by leaders of Africa's Great Lakes region in the Ethiopian capital Addis Ababa. REUTERS/Tiksa Negeri (ETHIOPIA - Tags: POLITICS CIVIL UNREST HEADSHOT)
Katika taarifa tofauti iliyotolewa jumatatu kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, Rwanda imelituhumu jeshi maalumu la ulinzi wa amani nchini Kongo kuwa linashirikiana na waasi wa Kihutu, wa kundi la FDLR, ambao wanahusishwa na mauaji ya kimbari ya Rwanda ya mwaka 1994. Jeshi hilo jipya lina mamlaka ya kupigana na kuwanyang'anya silaha waasi katika eneo la mashariki mwa Kongo.
Mpaka sasa walinzi hao wa amani 3,000 kutoka Afrika Kusini, Tanzania na Malawi

0 comments:

JESHI LA KONGO LASHAMBULIA WAASI MASHARKI MWA MJI WA GOMA

 A Congolese army soldier walks through the bush, back from an attack position north-west of Munigi, overlooking the front-line, in the east of the Democratic Republic of the Congo on July 15, 2013. Fighting broke out yesterday between M23 rebels and the national army, and continued today, with heavy artillery fire north-west of Munigi and the army claiming to have taken ground. AFP PHOTO/PHIL MOORE (Photo credit should read PHIL MOORE/AFP/Getty Images)
Majeshi ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo kwa kutumia helikopta yameyashambulia maeneo ya waasi karibu na upande wa mashariki mwa mji wa Goma, ikiwa siku ya tatu ya mapigano makali yaliyosabaisha wimbi la ukimbizi.
Katika barua ilitumwa kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ambayo Shirila la habari la Reuters limepata nakala yake, Kongo imekituhumu kikosi maalumu cha

0 comments:

MREMA AONYA VYAMA VENYE VIKUNDI YVA ULINZI ATA HATUA ZICHUKULIWE

Mrema aonya vyama vyenye vikundi vya ulinzi
MWENYEKITI wa Chama cha Tanzania Labour (TLP), Augustine Mrema amesema kitendo cha baadhi ya vyama vya siasa kuanzisha vikundi vya kujilinda ni sawa na kudhalilisha Jeshi la Polisi. Ametaka jeshi hilo lisidhoofishwe kulinda raia, mali zao na amani ya nchi kwa kuanzisha vikundi vya kufanya kazi hiyo.
Akizungumza na mwandishi wa habari hizi jana, ametaka vyama na wananchi kwa ujumla, washirikiane na Serikali kuimarisha jeshi litekeleze majukumu yake.
Mrema alionya kwamba yanayotokea Misri sasa, yanaweza kutokea nchini, ikiwa hatua za pamoja za kukabili changamoto zilizopo katika jamii hazitachukuliwa kwani

0 comments:

300 WATAPELIWA KUPEWA AJIRA JIJINI DODOMA

 300 watapeliwa kupatiwa ajira Dodoma
POLISI mkoani Dodoma inawashikilia watu wawili waliokuwa wakitapeli wananchi kwa kutoa vipeperushi vinavyoonesha nafasi za kazi mbalimbali za ajira kutoka kwa kampuni inayojulikana kama Granton Market Dubai (BJM).
Zaidi ya watu 300 mkoani Dodoma na mikoa mingine wanadaiwa kutapeliwa katika sakata la mlolongo wa kuahidiwa ajira; huku mmoja wao akitapeliwa Sh 400,000.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, David Misime, alisema kampuni hiyo haikusajiliwa na haitambuliki kisheria na baada ya upekuzi kufanyika katika nyumba iliyotumika kama

0 comments:

MIILI YA ASKALI WA JWTZ KULETWA JUMAMOSI NCHINI

 
Wakati miili ya wapiganaji hao ikiletwa, tayari familia zao zimeshawasili Dar es Salaam kwa ajili ya kuwapokea marehemu hao kwa maziko katika maeneo yaliyopangwa na wengine wakisubiri katika mikoa yao.
Dar/mikoani. Wakati miili ya askari wa Tanzania waliokufa Darfur ikitarajiwa kuletwa keshokutwa, ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu wameanza kuwasili Dar es Salaam kwa ajili ya kuipokea.
Msemaji wa Mpango wa Kulinda Amani wa Umoja wa Mataifa na Afrika (UNAMID), kwenye Mji wa Darfur, Chris Cycmakick alisema jana kuwa miili hiyo ilikuwa ikiendelea

0 comments:

SAM TIMBE AWAKOSOA WACHEZAJI WA BONGO KUSHINDWA KUWIKA SOKA LA KIMATAIFA

 
Kocha wa zamani Yanga, Sam Timbe amesema kukosekana kwa ushawishi na dhamira ya kufanikiwa kimataifa inayowazunguka wanasoka wengi nchini, kumeifanya Tanzania kushindwa kuwika katika soka la kimataifa.
Timbe, raia wa Uganda ambaye ni Kocha Msaidizi wa The Cranes,

0 comments:

''SPIKA MAKINDA ASIPUUZE USHAURI WA GAG'' MKAGUZI MKUU HESABU ZA SERIKALI (GAG)

 
Kwa mara nyingine, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Ludovick Utouh amemshauri Spika wa Bunge, Anne Makinda kubadili uamuzi wake na kuzirejesha kamati za Bunge za Mashirika ya Umma (POAC) na Hesabu za Serikali (PAC), akisema ilikuwa sio sahihi kuziunganisha kamati hizo kama alivyofanya.
Kumbukumbu zinaonyesha kuwa, mapema mwaka huu, Spika Makinda aliifuta POAC na kuunganisha shughuli zake na Kamati ya PAC, hatua ambayo kiongozi huyo wa CAG anasema ilikuwa ni makosa kwa sababu uamuzi huo usingeleta ufanisi katika kutekeleza majukumu ya ofisi yake ya kudhibiti na kukagua fedha za umma. Wakati Spika Makinda alipochukua hatua hiyo, CAG huyo alionyesha wasiwasi wake hadharani na kusema ungekuwa muujiza mkubwa iwapo

0 comments:

''KATIBA MPYA IPENDEKEZE SIKU ZA KUFANYA IBADA'' WAJUMBE WA HALMASHAURI YA WILAYA

 
Katika Mpya imependekezwa kuwa na kipengele chenye kuzitambua siku za ibada.
Mapendekezo hayo yalitolewa na wajumbe wa mabaraza ya kata wa Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe Vijijini wakati wa kikao kilichofanyika kwa siku tatu cha kuchambua na kujadili rasimu ya katiba iliyotolewa na Tume ya mabadiliko ya katiba.
Zuberi Mjata, kutoka Kijiji cha Kwagunda Wilayani hapa, alisema kwa kuwa ibara ya 31 katika eneo la Uhuru wa Imani ya Dini inasema kila mtu anao uhuru wa mawazo, imani na uchaguzi katika mambo ya ya imani ya dini, imani yake au kutokuwa na imani na dini.
Kipengele kisemacho kazi ya kutangaza dini, kufanya ibada na kueneza dini itakuwa

0 comments:

MAAFISA WA WIZARA YA FEDHA KIZIMBANI KWA TUHUMA ZA UFISADI WA FEDHA


Maofisa wawili wa Wizara ya Fedha wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu wakikabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi. Wanatuhumiwa kwa ufisadi wa fedha za utoaji wa matangazo na habari kwa vyombo mbalimbali vya habari.
Maofisa waliopandishwa kizimbani ni pamoja na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Ununuzi, Ernest Simon Mwakitalu na Ofisa Ununuzi, Liipu Neligwa ambao walisomewa mashtaka na Mwendesha Mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Leonard Swai.
Wakati maofisa hao wawili wakipandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka hayo, wengine wawili ambao walitakiwa kupandishwa kizimbani, Mkuu wa Kitengo cha Habari, Ingiahedi Mduma na Mkurugenzi wa Kampuni ya And- Line (2000) International, Daniel Ukwaya hawakuwapo mahakamani hivyo, mashtaka dhidi yao hayakusomwa hadi watakapokamatwa.
Washtakiwa hao wote kwa pamoja wanakabiliwa na jumla ya mashtaka 19. Shtaka moja ni kula njama kutenda kosa, mashtaka manane ya kutumia nyaraka za uongo ili kumdanganya mwajiri.
Mengine ni shtaka moja la matumizi mabaya ya madaraka, mashtaka manane ya kughushi, shtaka moja la ubadhirifu na shtaka moja la kusababisha hasara ya Sh19.8 milioni, ambalo ni shtaka mbadala kwa wote.
Akisoma hati ya mashtaka, Wakili Swai alisema washtakiwa hao walitenda makosa hayo kwa tarehe tofauti kati ya Juni na Julai, 2009.
Wakili Swai alidai kuwa washtakiwa hao walisaini hati za ununuzi zenye taarifa za uongo kwa lengo la kuonyesha kuwa Kampuni ya And Line (2000) International ilipewa fedha kwa ajili ya vipindi vinane vya matangazo katika vyombo vya habari vya redio, magazeti na runinga.
Alidai kuwa taarifa hizo kwenye vyombo vya habari zilihusu maonyesho ya 33 ya Biashara ya Kimataifa yaliyofanyika Dar es Salaam katika Viwanja vya Mwalimu Nyerere, Kilwa Road, kuanzia Juni 28 hadi Julai 10, 2009, kwa thamani ya Sh19.8 milioni, jambo ambalo si kweli.
Baada ya kuwasomea mashtaka, Wakili Swai alisema upelelezi wa kesi hiyo umekamilika na kuiomba Mahakama ipange tarehe nyingine ya kutajwa ambayo washtakiwe

0 comments:

''HAKIKA MANDELA NI NURU YA DUNIA YENYE HISIA KUBWA KWA BINADAMU'' DR SALIM AMESEMA

 
Aliyekuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU), Dk Salim Ahmed Salim amesema katika kipindi cha miaka saba alichofanya kazi na Rais wa Afrika Kusini, Nelson Mandela aligundua kuwa ni mtu muungwana na mwenye hisia kubwa kuhusu ubinadamu.
Dk Salim alisema jana katika mahojiano maalumu kuwa katika siku za mwanzo hakujiamini kufanya kazi na kiongozi huyo ambaye anatambuliwa kama nuru ya dunia.
Alisema alikutana kwa mara ya kwanza na Mandela Mjini Addis Ababa, Ethiopia mwaka 1990 alipokuwa mtendaji mkuu wa OAU ambapo Mandela alikatiza ziara yake

0 comments:

SHEREHE YA KUZALIWA YA MANDELA YAFANYIKI AHOSPITARINI MEDCLINIC

Kwa ufupi
Siku ya Mandela huadhimishwa kuenzi kazi za kiongozi huyo alizozifanya kwa miaka 67 akiutumikia umma wa wananchi wa Afrika Kusini, zikiwamo vita dhidi ya ubaguzi wa rangi na hatimaye kuwa Rais wa kwanza mzalendo kwa miaka mitano, kisha kustaafu.
Johannesburg: “Happy birthday Mzee Madiba.” Rais wa kwanza na mzalendo wa Afrika Kusini, Nelson Mandela, leo anatimiza umri wa miaka 95, pia anatimiza siku ya 40 tangu alipolazwa katika Hospitali ya Medclinic, Pretoria kwa ajili ya matibabu.
Nelson Rolihlahla Mandela, alizaliwa Julai 18, 1918 katika Kijiji cha Mvezo, eneo la Mthatha, Transkei Mkoa wa Eastern Cape na ametumia zaidi ya asilimia 70 ya maisha yake akipigania haki na usawa wa wananchi wa Afrika Kusini.
Maadhimisho ya miaka 95 tangu kuzaliwa kwa Mandela yanabeba uzito mkubwa kuliko maadhimisho mengine yaliyotangulia kwani kwa siku 40, wananchi wa Afrika Kusini wamekuwa katika wasiwasi mkubwa hasa kutokana na kuzorota kwa afya ya kiongozi huyo.
Mandela alilazwa katika hospitali hiyo Juni 8, mwaka huu akiugua magonjwa ya figo na afya yake imeelezwa kuwa ni mbaya.
Leo, Rais Jacob Zuma atawaongoza mamilioni ya wananchi wa Afrika Kusini katika maadhimisho ya nne ya kimataifa ya ‘Siku ya Mandela’ ambayo yanakwenda sambamba na siku yake hiyo ya kuzaliwa.
Tangu kulazwa kwa Mandela huko Pretoria, Rais Zuma amekuwa akiwahimiza wananchi wake wajiandae kusherehekea miaka 95 ya Mandela akiwatia moyo wale waliokuwa na wasiwasi

0 comments:

PICHA ZA MAANDAMANO YA AMANI YALIYOFANYWA NA CHADEMA KUELEKEA OFISI YA MKURUGENZI WA JIJI ARUSHA

Wafuasi wa CHADEMA wakishangilia ushindi katika maandamano ya amani ya madiwani wapya na viongozi kwenda kumpongeza Mkurugenzi wa jiji kwa kusimamia uchaguzi vizuri.,


Lema akiwa na madiwani wapya wakiingia katika

0 comments: