MIKAO KAMA HII HUCHANGIA HAMASA YA NGONO SEHEMU ZA KAZI HASA KWA MABOSI WANAOTUMIA VYEO VYAO KULAZIMISHA NGONO

 
  • Mabosi huwatafutia safari kama njia ya kuwanasa kwa kuwa wanapokuwa hotelini pekee, wanawake wengi wanakosa ujasili wa kukataa.
  • Wengine hutoa ofa kama vile kupandishwa vyeo, kununulia magari au hata safari za nje.Wengi wanaofanya haya ni waume za watu, wengine ukitajiwa ni ngumu kuamini kwa namna wanavyoonekana wana hekima usoni au mavazi yao.
Licha ya harakati mbalimbali za kumkomboa mwanamke, bado kuna mabosi nchini wanawanyanyasa wanawake kwa kuwalazimisha kufanya nao ngono.
Wapo wanaonyanyaswa au hata kuteswa ikiwemo kusemwa maneno machafu au kutishiwa kufukuzwa kazi kwa sababu tu wamekataa kutoa penzi kwa bosi.
Wale wanaokubali, wengine wanaishia
kupewa ahadi hewa za kufundishwa magari, kupelekewa kozi mbalimbali. Hata hivyo mbaya zaidi ni kwamba mabosi wengine hata kama wameoa, hupenda kuwamiliki wanawake hao kana kwamba ni wake zao kwa kuwafuatilia sana nyendo zao.
Ukahaba wa mabosi hufanywaje?
Baadhi ya wanaume kwa mwonekano ni vigumu kuamini kama ndiyo wanaofanya vitendo vichafu kwa wafanyakazi wao. Wanaposimama kwenye vikao, utasema mtu huyu, lakini wafanyakazi wa kike wamekuwa ni wenye kuwanyanyasa mno.
Baadhi ya mabosi wamekuwa wakitoa vitisho kuwa ‘kama hunipi penzi nitakuporomosha cheo au hata kukufanyia visa vyovyote hadi uhame’.
Katika baadhi ya ofisi badala ya mabosi kutumika kama washauri wa  wafanyakazi wao kuzipenda ndoa na nyumba zao, ndio wamekuwa wakitumia fedha zao kuwahonga wanawake hata magari, huku makatibu muhtasi wakidaiwa kuwa ndio wanaosumbuliwa zaidi.
Wapo mabosi huwaingia wanawake wakiwemo wake za watu kwa kuwapangia safari za mikoani au nje ya nchi hasa wanapoona hawana wepesi wa kukubaliana na matakwa yao.
“Nakumbuka kuna bosi mmoja katika ofisi moja nyeti aliwahi kudaiwa kumnunulia gari mke wa mtu kabla ya kuhama chombo hicho,” anasema mkazi mmoja wa Kimara.
Bosi aliweza kumpa safari ya nje mwanamke na kisha kumnunulia gari zuri kuliko la mumewe.
Hii ni moja ya kati ya matukio mengi ya mabosi kuwaingiza wafanyakazi wao katika ngono badala ya kuwa ndio washauri wema kwa wafanyakazi ili waweze kuziheshimu ndoa zao.
CHANZO MWANANCHI
Share on Google Plus

0 comments: